Baker alikuwa akifanya kazi katika Kituo cha Watoto yatima kinachoendeshwa na kituo cha msaada kutoka Uingereza.Kituo hicho kiko nje ya mji wa Freetown.
Watoto 33 na Wafanyakazi saba katika nyumba ya yatima St George, wamewekwa katika Karantini tangu Bwana Baker alipobainika kuwa na Virusi vya Ebola.
Kituo hiki kilianzishwa mwaka 2004 mpaka pale Ugonjwa wa Ebola ulipoingia, kituo kilijikita zaidi katika kuwaokoa Watoto wa mitaani.
Mwaka jana kituo kiliwasaidia Watoto takriban 200 walioachwa na familia kutokana na Ebola.
Ebola imeua zaidi ya Watu 9,500 nchini humo,Liberia na Guinea.
Lakini katika kipindi cha majuma ya hivi karibuni, kasi ya maambukizi ya Ugonjwa huu imepungua na Serikali za nchi tatu zimeahidi kumaliza kabisa tatizo hili ndani ya miezi miwili ijayo.
0 comments:
Post a Comment