TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Malema atishia kuvuruga hotuba ya Zuma

http://static.guim.co.uk/sys-images/Guardian/About/General/2012/2/4/1328382138749/Julius-Malema--007.jpg
 Chama cha siasa nchini Afrika Kusini kimetishia kuvuruga hutuba ya rais kwa taifa kikitaka Rais Jacob Zuma kuwajibika kuhusu ufisadi.
http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/01380/JacobZuma_1380559c.jpg
 The Economic Freedom Fighters inasema kuwa Zuma lazima aeleze nchi wakati anapanga kulipa fedha za umma zilizotumika katika nyumba yake binafsi.
Wananchi wa Africa Kusini hawatilii maanani hotuba ya nchi ya kila mwaka, kwa hivyo ni juu ya mapambo wala si umuhimu wake
Lakini mwaka huu, Mbunge machachari Julius Malema, ametishia kuvuruga hotuba ya rais Zuma.
Bwana Malema anasema rais lazima aeleze kwa nini amekataa kulipa fedha zilizotumika kwa kutengeneza nyumbani kwake katika kijiji cha Nkandla.
Malumbano yanatarajiwa na kuna uwezekano polisi wataitwa bungeni.
 http://www.kiswahili.rfi.fr/sites/kiswahili.filesrfi/dynimagecache/0/0/452/338/344/257/sites/images.rfi.fr/files/aef_image/Police%20have%20been%20caught%20up%20in%20the%20battles%20between%20workers%20and%20employers%20for%20weeks%20in%20South%20Africa.jpg
 Kwa miaka 20 chama tawala ANC kimekuwa kikisherehekea umaarufu wake wa kuwa na wanachama wengi.
Lakini Rais Zuma ameshindwa kutupilia mbali kashfa hio, na Wananchi wa Afrika Kusini wamekerwa na kudorora kwa uchumi na kwa upungufu wa nguvu za umeme kote nchini Hata hivyo baadhi ya wananchi, wanamtaja Bw Malema, na EFF, kuwa mtu anayetumia njia ovyo kupata umaruufu
Lakini wengine wanasema rais anafifisha demokrasia changa ya Afrika Kusini, na lazima kuwajibishwa.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)