TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Toure: Nimeua Afcon, bado EPL

http://www.africaguinee.com/sites/default/files/field/image/yaya.jpg
 Akizungumza mara baada ya kuiongoza timu yake ya taifa, Ivory Coasta, kutwaa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika juzi Jumapili usiku, Toure, ambaye alishutumiwa kwa kutojituma kwenye fainali hizo za Afcon, alisema sasa yupo fiti kurejea katika majukumu ya klabu.
http://taarifa.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/toure1.jpg
 YAYA Toure amewaambia wanasoka wenzake wa klabu ya Manchester City kuwa ni lazima wahakikishe wanashinda mechi zilizosalia za Ligi Kuu England kama kweli wanataka kutetea taji.
Akizungumza mara baada ya kuiongoza timu yake ya taifa, Ivory Coasta, kutwaa ubingwa wa Kombe la Mataifa ya Afrika juzi Jumapili usiku, Toure, ambaye alishutumiwa kwa kutojituma kwenye fainali hizo za Afcon, alisema sasa yupo fiti kurejea katika majukumu ya klabu.
Hata hivyo, kwa kuwa Man City ipo nyuma ya vinara Chelsea kwa pointi saba, staa huyo anakiri kwamba haitakuwa kazi rahisi kupindua mambo.
Toure, nahodha wa Ivory Coast iliyotwaa Afcon juzi kwa penalti 9-8 mbele ya Ghana, alisema: “Kwa uzoefu wangu nafahamu soka si mchezo wa mechi moja au mbili, hasa kwenye Ligi Kuu England.
“Tuna mechi 38 na kama tunataka kufanikiwa (kutetea ubingwa) tunapaswa kushinda michezo hiyo yote. Ninajua ni jambo gumu, lakini sasa nimemaliza majukumu ya timu ya taifa na ninarudi kuitetea klabu yangu.”
Mbele ya Ghana juzi, Toure, alifunga penalti yake katika fainali ambayo pia kipa Boubacar Barry naye alifunga kuhitimisha ushindi huo wa Ivory Coast.
Kuhusiana na shutuma dhidi yake alisema: “Hata ninapokuwa Manchester kuna watu huwa wananishutumu, kuhusu mambo mengi.
“Wakati fulani unapozungumza ukweli kuhusu soka, watu hawakusikilizi, hasa nyinyi (waandishi wa habari).
Badilikeni. Mara zote mimi ni mtu ninayepigania mafanikio ya timu, lakini ninajua naweza nisiheshimiwe kwa hilo, ndiyo soka lilivyo. Lakini kazi yangu ni kujituma uwanjani si kukatishwa tamaa na watu wanaoketi mbele ya TV zao na kusema wanayojisikia.”
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)