TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Al-Azhar yaasisi kituo cha elektroniki kupiga vita ugaidi

Sheykhul Azhar, Ahmed El Tayyib Chuo Kikuu cha Kiislamu cha al-Azhar nchini Misri, kimeasisi kituo cha elektroniki katika juhudi za kukabiliana na makundi yenye misimamo ya kufurutu ada na ya kigaidi. Abas Shuman, mmoja wa viongozi waandamizi wa al-Azhar amesema kuwa, mbinu za jadi za kuwafikia watu hazitoshi na ndio maana makundi yenye misimamo mikali yameamua kutumia Intaneti kueneza fikra zao na kwamba, kwa kuasisiwa kituo hicho cha elektroniki, kutasaidia kukabiliana na makundi hayo kupitia Intaneti. Shuman amesisitiza kuwa, kituo hicho kitatumika katika kuwazindua walimwengu kwamba, fikra za kitakfiri, kufurutu ada na ugaidi ni mambo yasiyo na nafasi kabisa katika Uislamu. Inaelezwa kuwa, kituo hicho kitatumika pia katika kuzifuatilia, kuzijibu na hata kuzizuia jumbe na fikra zinazotumwa na wanachama wa kundi la kitakfiri la Daesh kwa vijana. Hata hivyo Chuo Kikuu cha al Azhar kimetangaza kuwa, kituo hicho hakitahusika na mashambulizi yoyote ya kielektroniki dhidi ya vituo vingine vya Intaneti vinavyomilikiwa na makundi ya kigaidi na kitakfiri.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)