TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Mazungumzo ya amani Libya yamalizika

Mazungumzo ya amani Libya yamalizika Mazungumzo ya siku tatu ya kusaka amani baina ya makundi hasimu Libya  yamemalizika huku pande zote zikirejea katika ngome zao kwa ajili ya kufanya ushauriano.
Kwa mujibu wa taarifa ya Umoja wa Mataifa, pande hasimu zina azma ya kupunguza hitilafu zao ili kuwasilisha mapendekezo ya kimsingi ya kurejesha amani Libya.  Mazungumzo hayo yaliyomalizika jana Jumamosi katika mji wa Skhirat nchini Morocco yalijumuisha serikali mbili hasimu nchini Libya na alifanyika chini ya upatanishi wa mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa Bernardino Leon. Mazungumzo hayo yanatarajiwa kuendelea wiki ijayo.
Kuwepo serikali mbili na mabunge mawili kwa wakati mmoja nchini Libya kumesababisha hali ya mkanganyo na mchafukoge kuenea katika kila pembe ya nchi hiyo ya Afrika Kaskazini. Serikali ya kwanza ya Kongresi ya Kitaifa ina makao yake katika mji mkuu Tripoli na isiyotambuliwa kimataifa inaungwa mkono na wanagambo wa Fajr Libya. Serikali ya pili ni ile yenye makao yake mjini Tobruk ambayo inatambuliwa kimataifa. Hali ya usalama na kisiasa imezidi kuwa mbaya zaidi nchini Libya baada ya kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh kujiingiza ndani ya ardhi ya nchi hiyo na kuishikilia baadhi ya miji muhimu kama vile Sirte na Darna.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)