TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Simba yakamia nafasi ya tatu Ligi Kuu


http://wavuti.weebly.com/uploads/3/0/7/6/3076464/1359502_orig.jpg

SIMBA itacheza na Polisi MoroLeoJumapili kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro na kocha Goran Kopunovic amesema ni lazima waibuke na ushindi ili kujiweka pazuri kwenye msimamo wa Ligi Kuu Bara.
Kama ikishinda mchezo huo, timu yake hiyo inaweza kupanda hadi nafasi ya tatu.
Wakati Simba ikijiandaa na mchezo huo aliyekuwa kocha wao Mserbia Zdravko Logarusic amepewa ulaji mpya na sasa atainoa timu ya AFC Leopards ya Kenya.
Kocha huyo aliyetimuliwa na nafasi yake kukabidhiwa Mzambia Patrick Phiri ambaye naye ametimuliwa, jana alisaini mkataba wa miaka miwili na timu hiyo ya Kenya mbele ya Katibu Mkuu wa Leopards, George Aladwa na ataanza kuinoa timu hiyo wiki ijayo.
Akizungumzia mechi ya Jumapili kocha wa sasa wa Simba, Kopunovic alisema haijalishi anacheza kiwanja gani kwani aina ya soka analotaka vijana wake wacheze ni la kushambulia na kusaka ushindi kwa udi na uvumba na ndivyo itakavyokuwa katika mchezo huo na Polisi.
Kocha huyo wa zamani wa Polisi Rwanda alisema anatarajia kufanya mabadiliko machache kuhakikisha wanaibuka na ushindi mnono katika mechi hiyo ili kujiweka nafasi nzuri kwenye msimamo wa ligi unaoongozwa na Azam yenye pointi 25 sawa na Yanga inayoshika nafasi ya pili. “Napenda soka la kushambulia, hilo ndilo tutakalocheza keshokutwa (leo) Jumapili dhidi ya Polisi, hayo ndiyo maandalizi niliyowapatia wachezaji wangu,’’ alisema. “Sipendi kufanya mabadiliko mengi, tunaweza kuwa na mabadiliko machache kutoka kikosi kilichocheza na Coastal Union, labda moja ama mawili.”
Hata hivyo, Simba inaingia katika mchezo huo ikiwa inafasi ya tisa na pointi 17 baada ya kucheza michezo 13 na kushinda mitatu tu. Polisi wao wako nafasi ya tatu wakiwa na pointi 19 baada ya kucheza mechi 14 na kushinda nne pekee. Mechi ya mwisho iliyozikutanisha timu hizo ilimalizika kwa sare ya bao 1-1 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kocha wa Polisi Moro, Adolf Rishard alisema: “Tunafahamu kuwa tunakwenda kucheza na moja ya timu bora, mchezo wa Jumapili hautakuwa rahisi kwani si Simba ile tuliyocheza nayo kwenye mechi za mzunguko wa kwanza.”
Mechi nyingine inayochezwa jana Jumamosi ni kati ya Coastal Union na Mbeya City kwenye Uwanja wa Mkwakwani Tanga. Coasta iliingia uwanjani ikiwa nafasi ya saba na pointi 18 baada ya kucheza mechi 14 wakati Mbeya City wapo nafasi ya 10 na pointi 16 baada ya kucheza mechi 13.
Mechi tatu za mwisho zilizozikutanisha timu hizo, Mbeya City imeshinda mara mbili huku mchezo mmoja ukimalizika kwa sare.
Kocha wa Coastal, James Nandwa alisema: “Tumefanya mazoezi ya kufunga kwa wiki nzima hasa baada ya kugundua tuna upungufu huo.’’
Ofisa Habari wa Mbeya City, Dismas Ten alisema: “Kikosi kipo kwenye hali nzuri, hatuna majeruhi na tunatarajia kiungo Steven Mazanda aliyekosa mchezo wa mwisho kutokana na kadi za njano atarejea.’’
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)