TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Tanzania yakanusha kuwepo al Shabab eneo la Tanga

http://static.guim.co.uk/sys-images/Guardian/Pix/pictures/2013/10/9/1381314911680/Al-Shabaab-fighters-014.jpg 
 Afisa mwandamizi wa polisi nchini Tanzania amekanusha tetesi kuwa magaidi wa kundi la Al-Shabab wamekabiliana na vikosi vya usalama katika eneo la Tanga. Kamishna wa Oparesheni katika jeshi la Polisi CP Paul Chagonja amenukuliwa na vyombo vya habari akisema jana  kuwa askari wawili wa jeshi la polisi na askari wanne wa jeshi la wananchi Tanzania JWTZ wamejeruhiwa vibaya kwa risasi baada ya kutokea mapigano kati yao na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi katika mapango ya Amboni mkoani Tanga.
Akitoa taarifa rasmi ya jeshi la polisi kuhusiana na tukio hilo jana Jumamosi, Chagonja amethibitisha kutokea kwa tukio hilo siku ya Ijumaa ambapo amesema kuwa si tukio kubwa kama linavyoelezwa na baadhi ya watu na kwamba waliohusika ni majambazi na siyo magaidi. Amesema kilichotokea ni oparesheni ya kawaida iliyofanywa na jeshi la polisi kuwasaka watu wanaosadikiwa kuwa majambazi waliodaiwa kujificha katika mapango hayo na ndipo yalipotokea mapigano hayo yaliyoambatana na kurushiana risasi na kupelekea askari hao kujeruhiwa.
Amesema baada ya hali kuwa tete, jeshi hilo lililazimu kuomba msaada kutoka kwa askari wa jeshi la wananchi Tanzania JWTZ ambao walifika katika eneo la tukio na kufanikiwa kutuliza hali ya taharuki iliyokuwa imetanda katika eneo hilo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)