Msikiti wa Hamou al-Qadu ulibomolewa kikamilifu na magaidi wa Daesh ambao pia wamebomoa idadi kubwa ya misikiti na maeneo mengine ya kidini a yakatika maeneo kadha Iraq na nchini Syria. Msikiti uliobomolewa ulijengwa mwaka wa 1880 Miladia katika zama za utawala wa Othmaniya. Mwezi uliopita pia magaidi hao wa Kiwahabi walibomoa msikiti wa kale zaidi katika mkoa wa Al Anbar nchini Iraq. Kundi la kigaidi la Daesh (ISIL, ISIS au IS) linadhibiti baadhi ya maeneo ya Syria na Iraq. Kundi hilo lilianzisha kampeni ya ukatili nchini Iraq mnamo Juni 2014 wakati magaidi wa kundi hilo walipovamia na kuuteka mji wa Mosul. Magaidi hao wametekeleza jinai za kinyama dhidi ya Masunni, Mashia, Wakurdi na Wakristo katika maeneo hayo. Serikali ya Iraq inazituhumu baadhi ya nchi jirani kuwa ndizo zinazounga mkono kundi la Daesh. Serikali ya Syria nayo imeitaja Marekani na waitifake wake katika eneo yaani utawala wa Kizayuni wa Israel, Saudi Arabia, Qatar na Uturuki kuwa ndio waungaji mkono asili wa magaidi wa Daesh.
Daesh (ISIL) wabomoa misikiti zaidi mjini Mosul, Iraq
Msikiti wa Hamou al-Qadu ulibomolewa kikamilifu na magaidi wa Daesh ambao pia wamebomoa idadi kubwa ya misikiti na maeneo mengine ya kidini a yakatika maeneo kadha Iraq na nchini Syria. Msikiti uliobomolewa ulijengwa mwaka wa 1880 Miladia katika zama za utawala wa Othmaniya. Mwezi uliopita pia magaidi hao wa Kiwahabi walibomoa msikiti wa kale zaidi katika mkoa wa Al Anbar nchini Iraq. Kundi la kigaidi la Daesh (ISIL, ISIS au IS) linadhibiti baadhi ya maeneo ya Syria na Iraq. Kundi hilo lilianzisha kampeni ya ukatili nchini Iraq mnamo Juni 2014 wakati magaidi wa kundi hilo walipovamia na kuuteka mji wa Mosul. Magaidi hao wametekeleza jinai za kinyama dhidi ya Masunni, Mashia, Wakurdi na Wakristo katika maeneo hayo. Serikali ya Iraq inazituhumu baadhi ya nchi jirani kuwa ndizo zinazounga mkono kundi la Daesh. Serikali ya Syria nayo imeitaja Marekani na waitifake wake katika eneo yaani utawala wa Kizayuni wa Israel, Saudi Arabia, Qatar na Uturuki kuwa ndio waungaji mkono asili wa magaidi wa Daesh.
0 comments:
Post a Comment