TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Wananchi Jordan wapinga mkataba wa gesi na Israel

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/4ef453601d616e9c9ab8180a8d295af0_XL.jpgWananchi wa Jordan wamefanya maandamano mjini Amman dhidi ya utawala haramu wa Kizayuni wa Israel. Katika maandamano hayo washiriki wamelaani mkataba wa gesi baina ya nchi yao na utawala wa Kizayuni na wametaka kukomeshwa mkataba huo mara moja. Aidha wamesisitiza kwamba Jordan haipaswi kushirikiana kwa aina yoyote na Israel katika ununuzi wa gesi kwa kuwa gesi hiyo ni mali halali ya Wapalestina. Wameongeza kuwa, fedha za mauzo yatokanayo na gesi hiyo zinatumiwa na Tel Aviv katika kuwaua Wapalestina wasio na hatia wala ulinzi. Aidha waandamanaji wameitaja Israel kuwa ndiye adui wa Waarabu na Waislamu kwa ujumla. Aidha waandamanaji hao wameitaka serikali ya Amman kuangalia njia mbadala ya kudhamini nishati yake kwa kuwa nchi hiyo inamiliki vyanzo vingi vya utajiri hususan katika sekta ya nishati. Maandamano hayo yalifanyika jana Ijumaa chini ya ulinzi mkali wa askari wa nchi hiyo. Hii si mara ya kwanza kwa raia wa Jordan kufanya maandamano kama hayo katika kulalamikia mahusiano yaliyopo kati ya viongozi wa serikali ya Amman na Israel na kutaka kukomeshwa ushirikiano wowote na utawala huo uliotapakaa damu za ndugu zao Wapalestina.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)