TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Wasi wasi wa Umoja wa Mataifa kuhusu jamii ya kimataifa kupuuza haki za wanawake

Bi. Phumzile Mlambo-NgcukaKadhia ya kutozingatiwa uadilifu kwa wanawake na jamii ya kimataifa kwa mara nyingine, imeitia wasi wasi Umoja wa Mataifa. Phumzile Mlambo-Ngcuka, mkuu wa wakala wa masuala ya wanawake, ambao unasimamiwa na Umoja wa Mataifa amezungumzia suala hilo na kusema, licha ya kupita miaka 20 tangu kupasishwa sheria ya uadilifu kwa ajili ya wanawake huko Beijing, nchini China, kwa kuhudhuriwa na wajumbe wa nchi 189, lakini hadi sasa hakuna nchi iliyotekeleza ipasavyo sheria hiyo. Sanjari na kuonyesha wasi wasi wake kuhusiana na kukosekana uadilifu wa kijinsia katika nchi tofauti za dunia, Mlambo-Ngcuka amesema kuwa, wanawake wana fursa chache zaidi ikilinganishwa na wanaume, katika kupata ajira muhimu na nafasi za usimamizi katika jamii. Ngcuka ameongeza kuwa, mashinikizo mbalimbali ya kijamii na unyanya saji wa familia dhidi ya wanawake, ni tatizo la dunia na kwamba chanzo cha hali hiyo ni kukosekana usimamizi bora wa haki za binaadamu na uadilifu kwa wanawake katika jamii hizo. Afisa huyo wa Umoja wa Mataifa ameyasema hayo ikiwa zimesalia siku mbili tu kabla ya kufanyika sherehe za ‘Siku ya Wanamke Duniani’ ambazo zimepangwa kufanyika tarehe nane ya mwezi huu na pia kikao cha wiki ijayo cha tume inayoshughulikia hali ya wanawake katika nchi tofauti dunia. Amesema kuwa, njia pekee ya kupunguza uhalifu wa kijinsia na kukosekana uadilifu wa kijamii dhidi ya wanawake ni kufanywa juhudi za dhati na viongozi wa dunia kwa ajili ya kukabiliana na vitendo hivyo. Siku chache zilizopita pia kulifanyika kikao cha taasisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia masuala ya wanawake huko nchini Chile ambapo kulisisitizwa udharura wa kuhitimishwa ubaguzi dhidi ya wanawake. Katika ripoti iliyotolewa na kikao hicho chini ya kauli mbiu ya ‘Wito kwa ajili ya Utekelezaji’ Ban Ki-Moon, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Michelle Bachelet Rais wa Chile waliutaja mwaka 2015, kuwa mwaka wa kupambana na ubaguzi kati ya wanawake na wanaume na kufuatilia uadilifu wa kijinsia duniani, sanjari na kumtaka kila mtu kufanya juhudi kwa ajili ya kufanikisha lengo hilo. Aidha imepangwa katika vikao vijavyo vya viongozi wa Umoja wa Mataifa, kujadiliwa ripoti yenye kurasa 150 juu ya udhaifu uliopo katika utekelezaji wa malengo ya uadilifu wa kijinsia, kuhusu ripoti iliyotiwa saini mwaka 1995 mjini Beijing nchini China. Katika kongamano la mjini Beijing, viongozi wa nchi kadhaa za dunia, walitakiwa kufanya juhudi za kupunguza ubaguzi wa kijinsia dhidi ya wanawake na pia kuondoa vizingiti vya ukosefu wa usawa sanjari na kupiga hatua 12 mbele za utekelezaji ikiwemo, afya, elimu, ajira, ushiriki wa kisiasa na pia haki za binaadamu. Hata hivyo na licha ya kupita miaka 20 tangu kufanyika kikao hicho, uchunguzi wa maoni unaonyesha kwamba, asilimia kubwa ya wanawake duniani sanjari na kuteseka, wanakumbana pia na matatizo mengi ya kimaisha. Taasisi ya Gallup inayojishughulisha na uchunguzi wa maoni, hivi karibuni ilitangaza kuwa, zaidi ya wanawake bilioni mbili, wanaishi maisha yenye matatizo mengi. Uchunguzi huo uliofanywa katika zaidi ya nchi 160 za dunia, unaonyesha kwamba, ni wanawake milioni 620 pekee ndio wanaoishi katika mazingira yanayoweza kustahmilika ya kimaisha. Aidha uchunguzi wa wataalamu wa Umoja wa Mataifa unaonyesha kwamba, kukosekana mfumo wa sheria, kunatajwa kuwa sababu ya  ongezeko la vitendo vya ukosefu wa uadilifu, ubaguzi, unyanyasaji wa kifamilia, ukandamizaji wa kijinsia, magendo ya binaadamu kwa kuuzwa wanawake na wasichana, ndoa za lazima za utotoni, kukithiri wanawake wa mitaani, na aina nyingine ya ukatili dhidi ya wanawake unaoshuhudiwa katika nchi mbalimbali duniani.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)