TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Nigeria: Tunazidi kupata ushindi dhidi ya Boko Haram

Nigeria: Tunazidi kupata ushindi dhidi ya Boko Haram Jeshi la Nigeria limetangaza kuwa, linaendelea kupata ushindi katika vita vyake dhidi ya kundi la Boko Haram na hadi sasa limefanikiwa kuteka kiwango kikubwa cha silaha za kundi hilo ambalo limekimbia katika mji wa Baga baada ya kuzidiwa nguvu na jeshi. Msemaji mmoja wa jeshi la Nigeria amethibitisha habari hiyo na kuongeza kuwa, jeshi la Nigeria hivi sasa linaendesha operesheni ya kuuzingira na kuwasaka wanamgambo wa Boko Haram katika mji wa Baga na limefanikiwa kukamata silaha nyingi zilizoachwa nyuma na wanamgambo hao ambao wanaendelea kukimbia huku na huko. Mji wa Baga ni moja ya maeneo muhimu ya uvuvi katika fukwe za Ziwa Chad, kaskazini mwa jimbo la Borno la kaskazini mashariki mwa Nigeria. Mji huo ulikombolewa kutoka mikononi mwa wanamgambo wa Boko Haram juzi Jumamosi. Kundi la Boko Haram ambalo lina welewa finyu kuhusu mafundisho ya dini tukufu ya Kiislamu lilianzisha mashambulio ya kigaidi katika maeneo mbalimbali ya Nigeria mwaka 2009, na limetangaza kuhusika katika utegaji mabomu, ufanyatuaji risasi, mashambulizi ya kutisha na jinai mbalimbali ndani ya Nigeria na katika nchi jirani. Zaidi ya watu 13 elfu wamesharipotiwa kuuawa hadi hivi sasa na milioni moja na nusu wengine kuwa wakimbizi kutokana na mashambulio hayo ya Boko Haram.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)