TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Jonathan: Ni uhaini kuasisi serikali ya muda Nigeria

Rais Jonathan Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria amesema kuwa ni uhaini kwa yoyote kufanya njama ya kutaka kuasisi serikali ya muda nchini Nigeria. Rais wa Nigeria ameyasema hayo Jumapili hii huko Abuja mji mkuu wa nchi hiyo katika mkutano na Maaskofu wa Katoliki wa Nigeria. Rais Goodluck wa Jonathan ameyasema hayo siku kadhaa baada ya Rais wa zamani wa nchi hiyo Olusegun Obasanjo kudai kuwa Rais Jonathan anapanga kufanya udanganyifu katika uchaguzi au kusababisha mgogoro ili asalie madarakani. Hata hivyo Rais Jonathan amesema kuwa ana imani kuwa Nigeria itaendelea kuwa tulivu na kusisitiza kwamba uongozi wa muda nchini humo pia ni kinyume cha katiba. Reuben Abati, Msemaji wa Rais wa Nigeria hivi karibuni alimtuhumu Rais wa zamani wa nchi hiyo Olusegun Obasanjo kuwa anafanya njama na wengine ili kuchochea mgogoro na kuasisi serikali ya muda nchini Nigeria.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)