TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Maaskofu CAR: Anti-Balaka wapokonywe silaha

Maaskofu CAR: Anti-Balaka wapokonywe silaha Maaskofu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati, wametaka wanamgambo wa Kikristo wa Anti-Balaka wapokonywe silaha kwa lengo la kurejesha usalama nchini humo.
Taarifa iliyotolewa na maaskofu hao pia imelaani vitendo vya ukatili vinavyofanywa na wanamgambo hao kwa kutumia jina la Ukristo. Imeongeza kuwa, kabla ya Anti-Balaka kutekeleza pendekezo la Umoja wa Mataifa la kuwalinda raia, wanatakiwa kuweka chini silaha zao kwa hiari na kushiriki katika mchakato wa serikali katika kurejesha usalama na utulivu nchini.
Kwa mujibu wa azimio nambari 2149 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, kuanzia mwezi Julai mwaka huu, kutaanza operesheni kali ya kuyapokonya silaha kwa nguvu makundi ya waasi nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Mapigano baina ya waasi wa zamani wa Seleka na kundi la Kikristo la Anti-Balaka yalianza mwishoni wa mwaka 2012, na kusababisha mauaji ya maelfu ya watu na wengine kuwa wakimbizi wengi wao wakiwa Waislamu.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)