TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

LEO KATIKA HISTORIA Jumatatu, Februari 23

Jumatatu, Februari 23, 2015Leo ni Jumatatu tarehe 4 Mfunguo Nane Jamadul Awwal mwaka 1436 Hijria, mwafaka na tarehe 23 Februari mwaka 2015 Miladia.
Siku kama ya leo miaka mitano iliyopita Abdulmalik Rigi kiongozi wa kundi la kigaidi la Jundullah lenye makao yake huko Pakistan, alitiwa mbaroni katika oparesheni tata ya kiintelijinsia iliyofanywa na maajenti wa Wizara ya Usalama wa Ndani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Baada ya kufanya mashambulizi mengi ya kigaidi, gaidi huyo katili alikuwa safarini kuelekea nchini Kyrgyzstan akitokea Dubai, Imarati, kwenda kukutana na kufanya mazungumzo na kiongozi mmoja wa ngazi ya juu wa Marekani. Hata hivyo wana usalama wa Iran waliokuwa wakifuatilia kwwa karibu nyendo zake waliweza kuitambua ndege iliyokuwa imembeba gaidi huyo na kuisubiri iingie katika anga ya Iran na hivyo kuilazimisha kutua katika uwanja wa ndege wa Bandar Abbas wa kusini mwa Iran na baadae wakamtia mbaroni kiongozi huyo wa kundi la kigaidi la Jundullah. Rubani wa ndege hiyo alifanya jitihada kubwa za kutoroka na kutoka nje ya anga ya Iran, lakini alizidiwa nguvu na maafisa usalama wa Iran, na kulazimishwa kuishusha chini ndege hiyo kabla haijaingia kwenye anga ya Imarati. Abdulmalik Rigi alifanya jinai nyingi ikiwa ni pamoja na kutega na kuripua mabomu katika maeneo ya umma nchini Iran, kuwauwa kwa umati raia pamoja na kuwateka nyara. Rigi hakuwa na huruma hata kwa watu wake wa karibu. Abdulmalik Rigi alikiri kwamba alikuwa anapata misaada ya kila namna ikiwemo ya kifedha na kisilaha kutoka kwa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kama njia ya kuliwezesha kundi lake lifanye mauaji ya watu ndani ya Iran hususan katika maeneo ya kusini mashariki mwa Iran na kusababisha mizozo ya kimadhehebu katika maeneo hayo. Gaidi huyo alinyongwa tarehe 30 Khordad mwaka 1389 Hijria Shamsia sawa na tarehe 20 Juni, 2010 Milaadia yaani miezi minne baada ya kutiwa mbaroni. Kukiri huko kwa Rigi kunaonyesha wazi madai ya uwongo ya serikali ya Marekani ya eti inapambana na ugaidi.
*******
Siku kama ya leo miaka 129 iliyopita, Charles Martin Hall, mvumbuzi na mwanakemia wa Marekani alifanikiwa kuvumbua njia mpya ya upatikanaji wa aluminiamu. Aluminiamu ni chuma cheupe na chepesi kinachoweza kukunjwa kwa urahisi. Aluminiamu hiyo ambayo ni nyepesi kuliko chuma, leo hii imekuwa na matumizi mengi katika shughuli za viwanda na kadhalika.
*******
Siku kama ya leo miaka 216 iliyopita, Napoleon Bonaparte mfalme wa Ufaransa, alianza kuishambulia Sham, ambayo wakati huo ilikuwa ikiundwa na nchi za Syria, Jordan, Lebanon na Palestina. Mashambulio ya Bonaparte dhidi ya Misri yalifanyika kwa lengo la kutoa pigo kwa Uingereza iliyokuwa mkoloni wa Misri. Sababu ya mashambulio ya Napoleon Bonaparte dhidi ya Sham iliyokuwa sehemu ya ardhi ya utawala wa Othmania, ilikuwa ni hatua ya mfalme wa utawala wa Othmania ya kutangaza vita dhidi ya Ufaransa. Katika mashambulio hayo, na licha ya kwamba awali Bonaparte alipata ushindi, lakini baadaye alilazimika kuacha vita na kurejea kwao kutokana na uungaji mkono wa Uingereza na Urusi kwa utawala wa Othmania bila kusahau kuharibika hali ya mambo ndani ya Ufaransa.
*******
Na siku kama ya leo miaka 65 iliyopita, alifariki dunia Haidar Qali Khan Afghani, maarufu kwa jina la Sardor Kabili, msomi mkubwa wa Kiislamu. Alikuwa mtaalamu mkubwa wa elimu kama vile hisabati, nyota, historia, jiografia, falsafa, mantiki na fasihi ya lugha ya Kiarabu. Sardor Kabuli alikuwa na mapenzi makubwa na watu wa kizazi cha Bwana Mtume Muhammad (saw) na aliandika kitabu kilichoelezea fadhila za Imam Ali (as). Msomi huyo ameacha vitabu mbalimbali moja wapo kikiwa kitabu cha ‘Sharhu Duaye Nudbeh’ na ‘Munadharaat’.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)