TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

EU: Kuna wasiwasi wa kuzuka machafuko Burundi

EU: Kuna wasiwasi wa kuzuka machafuko Burundi Umoja wa Ulaya umeelezea wasiwasi ulionao kutokana na juhudi za chama tawala nchini Burundi za kutaka kubakia madarakani na uwezekano wa kutokea mivutano na machafuko katika nchi hiyo.
Patrick Spirlet, mwakilishi wa Umoja wa Ulaya nchini Burundi amesema hayo akiwa mjini Bujumbura na kusisitiza kwamba, kusimama Rais Pierre Nkurunziza kwa ajili ya kugombea katika uchaguzi ujao wa Rais ni hatari na kunaweza kuitumbukiza nchi hiyo katika mgogoro mkubwa na machafuko.
Mwakilishi huyo wa Umoja wa Ulaya nchini Burundi ameashiria malalamiko ya wananchi dhidi ya hatua ya kugombea tena Nkurunziza katika uchaguzi ujao na kusema kuwa, kwa mtazamo wa Umoja wa Ulaya kugombea Nkurunziza kwa mara ya tatu kunaweza kuitumbukiza Burundi katika mivutano na machafuko na hatimaye nchi hiyo kukabiliwa na hatari.
Hatua ya Rais Pierre Nkurunziza ya kutangaza nia yake ya kuwania tena kiti cha urais, imekabiliwa na malalamiko mengi nchini Burundi zikiwemo asasi za kiraia, wapinzani wa serikali na kanisa katoliki. Uchaguzi wa Rais nchini Burundi umepangwa kufanyika mwezi Juni mwaka huu.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)