TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Kamanda wa ngazi ya juu wa Daesh auliwa Libya

Kamanda wa ngazi ya juu wa Daesh auliwa Libya Mmoja wa wanamgambo wa Tunisia aliyekuwa akisakwa kwa udi na uvumba ambaye pia ni kamanda wa ngazi ya juu wa kundi la kigaidi la Daesh ameuawa katika mapigano nchini Libya. Mohammed Ali Aroui, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Tunisia amesema kuwa kifo cha kamanda huyo wa Daesh kwa jina la Ahmed al Rouissi kimethibitishwa kupitia njia za kitaalamu ambazo zilitumiwa kwa kushirikiana na maafisa wa Libya. Mwanachama huyo wa kundi la Daesh aliuliwa kwenye mapigano katika mji wa pwani wa Sirte kati ya kundi hilo na wapiganaji watiifu kwa kundi linaloudhibiti mji mkuu Tripoli lenye makao yake katika mji wa Misrata. Kamanda wa ngazi ya juu wa Daesh aliyeuliwa huko Libya anaaminika kuwa ndiye aliyekuwa akipanga mashambulizi mengi ya kigaidi huko nchini Tunisia yaliyokuwa yakitekelezwa na kundi la Kisalafi na lile la Ansarul Sharia, yakiwemo mauaji ya wanasiasa wa nchi hiyo Chokri Belaid na Mohamed Brahmi.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)