TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Jeshi lashambulia BH kuelekea uchaguzi Nigeria

Jeshi lashambulia BH kuelekea uchaguzi Nigeria Nigeria imesema kuwa imeanzisha shambulio la mwisho dhidi ya wanamgambo wa kitakfiri wa Boko Haram kabla ya kufanyika uchaguzi wa Rais tarehe 28 mwezi huu. Mike Omeri, msemaji wa serikali ya Nigeria amesema kuwa vikosi vya nchi hiyo vinafanya bidii kubwa na kwamba wanaelekea katika mashambulio ya mwisho dhidi ya Boko Haram, kwa sababu tayari wameshaanzisha oparesheni kuanzia huko Bama katika jimbo la Borno. Amesema kuwa mji wa Bama ulikombolewa juzi na kwamba maeneo ambayo bado hayajakombolewa ni Abadam, Gwoza na Askira. Msemaji wa serikali ya Nigeria ameongeza kuwa mafanikio makubwa ya kistratejia yamepatikana dhidi ya wanamgambo wa Boko Haram katika wiki za hivi karibuni. Mji wa Bama ulikuwa ukishikiliwa na Boko Haram tangu mapema mwezi Septemba mwaka jana wakati ulipodhibitiwa na kundi hilo pamoja na miji na vijiji kadhaa katika majimbo ya Borno, Adamawa na Yobe katika mpaka wa nchi hiyo na Chad, Cameroon na Niger. Jeshi la Nigeria huku likisaidiwa na Chad, Niger na Cameroon limekuwa likifanya oparesheni tafauti katika miezi ya hivi karibuni ili kurejesha utulivu katika maeneo ya kaskazini mashariki mwa nchi kabla ya kufanyika uchaguzi wa Rais.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)