TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Marekani yapunguza misaada ya kijeshi na kijasusi kwa Nigeria

Marekani yapunguza misaada ya kijeshi na kijasusi kwa NigeriaSerikali ya Marekani imetangaza kupunguza misaada yake ya kijeshi na kijasusi kwa Nigeria. Wakuu wa Marekani hivi karibuni walisema kuwa wanakata misaada hiyo kutokana na ukikwaji wa haki za binaadamu nchini Nigeria. Hali kadhalika wakuu wa Marekani wanadai kuwa Nigeria inatumia habari za kijasusi inazopata kukabiliana na makundi mengine badala ya Boko Haram. Serikali ya Nigeria imelaani hatua hiyo ya Marekani na kusema uamuzi huo wa Washington umekuja wakati nchi hiyo inahitajia sana msaada wa kijasusi.
Weledi wa mambo wanaamini kuwa, kuendelea harakati za Boko Haram katika hali ya hivi sasa nchini Nigeria ni kwa maslahi ya  baadhi ya serikali na ni kwa sababu hii ndio  nchi kama Marekani, huku zikijionyesha kama wapinzani wa  ugaidi, zikaandaa mazingira ya kuendelea harakati za kundi hilo la kigaidi.
Kwa kuzingatia uwezo mkubwa walionao magaidi wa Boko Haram hasa kwa mtazamo wa wapiganaji, zana za kivita na uwezo wa kiufundi na kilojistiki ni wazi kuwa Boko Haram wanapata himaya ya kigeni kwa malengo maalumu. Kuidhoofisha serikali ya Nigeria kama dola lenye nguvu Afrika na kuifanya ishughulike tu na mgogoro wa ndani ya nchi ni moja kati ya malengo ya Marekani. Hivi sasa gharama za kijeshi na kiusalama zimechukua sehemu kubwa ya bajeti ya Nigeria. Hii ni katika hali ambayo aghalabu ya watu wa Nigeria wanaishi kwa pato la chini ya dola mbili kwa siku katika hali ambayo nchi hiyo ina utajiri mkubwa sana wa mafuta na gesi. Katika upande mwingine, ukosefu wa usalama na mgogoro wa ndani ya Nigeria unaongozwa kwa njia maalumu ili kuhakikisha sekta za mafuta na gesi nchini humo haziathiriki. Hii ndio sababu tunashuhudia hujuma za Boko Haram zikiwa katika eneo la Kaskazini mwa Nigeria na si eneo la kusini lenye utajiri wa mafuta. Sababu ya jambo hili ni kuhifadhi vyanzo vya nishati Nigeria  ili mbali na Marekani , nchi za Ulaya ziendelee kupora utajiri wa nchi hiyo huku serikali ya nchi hiyo ikijishughulisha na mgogoro wa ndani.
Kuendelea harakati za Boko Haram pia kuna umuhimu mwingine kwa nchi za Magharibi. Kuenea fikra potofu za Boko Haram bila shaka kutapelekea kuchafuliwa sura ya Waislamu na Uislamu duniani. Nukta hii ni muhimu kwa vyombo vya habari na watawala wa nchi za Magharibi ambao wanataka kuendeleza sera zao za chuki dhidi ya Uislamu. Kuathiri mchakato wa uchaguzi nchini Nigeria ni lengo jingine la madola ya kibeberu katika kuunga mkono kwa njia isiyo ya moja kwa moja ugaidi wa Boko Haram. Uchaguzi wa rais nchini Nigeria unatazamiwa kufanyika katika kipindi cha wiki chache zijazo. Kwa hivyo kuibua vita na machafuko katika maeneo ya kaskazini yenye wakaazi wengi Waislamu hasa eneo la Kaskazini Mashariki kutapelekea Waislamu wapate matatizo katika upigaji kura na yamkini wasiweze kumpigia kura mgombea wanayemtaka. Nchi za Magharibi zinatumai kuwa, kuchaguliwa tena rais Mkristo nchini Nigeria kutavunja ile desturi ya kubadilishana uongozi baina ya Mwislamu na Mkristo katika nchi hiyo kubwa ya Magharibi mwa Afrika. Rais wa sasa wa Nigeria, Goodluck Jonathan ni Mkristo kutoka eneo lenye utajiri wa mafuta la Kusini. Kwa mujibu wa sheria ambayo haijaandikwa Nigeria, baada ya kumalizika muhula wa kisheria wa rais Mkristo rais anayefuata anapaswa kuwa Mwislamu.

Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)