TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Mkapa: Wanasiasa hawauelewi vizuri uwekezaji

Mkapa: Wanasiasa hawauelewi vizuri uwekezajiBenjamin William Mkapa Rais mstaafu wa Tanzania amesema kuwa, sekta ya uwekezaji nchini humo inashindwa kukua kwa kasi kama inayotarajiwa kutokana na baadhi ya wanasiasa kushindwa kuielewa vizuri. Akizungumza wakati wa kusaini makubaliano ya kusaidia kuvutia na kuongeza uwekezaji wa ndani na nje nchini kati ya Taasisi inayoshughulikia Mazingira ya Uwekezaji Barani Afrika ICF na Kituo cha Uwekezaji nchini Tanzania TIC, Mkapa ambaye pia ni Mwenyekiti mwenza wa ICF alisema kuwa, baadhi ya watu wanautazama uwekezaji kama unyonyaji. Chini ya makubaliano hayo, ICF itakisaidia kituo cha uwekezaji nchini katika kukuza, kuinua na kulitangaza dirisha la uwekezaji na kuimarisha uwezo wake katika kuwezesha na kufuatilia uwekezaji nchini Tanzania. Naye Mwenyekiti mwenza wa ICF Neville Isdell alisema kuwa, uwekezaji unahitaji uwazi ili kuwavutia wafanyabiashara wa ndani na nje kuendelea kuwekeza.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)