TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Niger yawazuia kabisa magaidi wa Boko Haram

Magaidi wa Boko HaramSerikali ya Niger imesema magaidi wa kundi la kitakfiri la Boko Haram hawawezi tena kuchukua udhibiti wa eneo lolote nchini humo.
Waziri Katika Ofisi ya Rais nchini Niger Mohammad Bazoum amesema nchi yake imedhibiti hali ya mambo na kwamba magaidi wa Boko Haram hawawezi tena kuchukua udhibiti wa mji wowote. Siku ya Jumatano msemaji wa pilisi nchini Niger Kepteni Adili Toro alisema tokea Februari mwaka 2015, nchi yake imeangamiza magaidi wapatao 500 wa Boko Haram kutoka nchi jirani ya Nigeria. Mnamo Machi 8 Chad na Niger zilianzisha oparesheni ya pamoja ya kijeshi dhidi ya magaidi wa Boko Haram kama sehemu ya jitihada za kieneo za kuangamiza kundi hilo la kitakfiri lenye makao yake kaskazini mwa Nigeria.
Neno Boko Haram kwa ya lugha ya Kihausa lina maana ya 'elimu kutoka nchi za Magharibi ni haramu'. Zaidi ya watu elfu 13 wamepoteza maisha nchini Nigeria tokea kundi la Boko Haram lianzishe uasi mwaka 2009. Boko Haram ni kundi lenye misimamo ya kufurutu mipaka nchini Nigeria ambalo kutokana na kuwa na ufahamu mbaya na potofu kuhusiana na Uislamu, limeitumbukiza nchi hiyo katika dimbwi la machafuko na mauaji sambamba na kuzusha hitilafu za kidini na kikabila nchini humo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)