TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Obama arefusha vikwazo kwa Zimbabwe, UK yalegeza

Obama arefusha vikwazo kwa Zimbabwe, UK yalegeza Rais Barack Obama wa Marekani amerefusha vikwazo dhidi ya Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe na watu wake wa karibu, huku serikali ya Uingereza ikimtuma Zimbabwe Waziri wake wa Maendeleo ya Kimataifa kwa ajili ya mazungumzo na utawala wa Harare.  Chama tawala cha Zimbabwe Zanu-pf kimelaani hatua hiyo ya Rais wa Marekani ya kurefusha muda wa vikwazo dhidi ya Rais Mugabe na watu wake wa karibu. Obama amesema kuwa tishio lililotokana na vitendo na sera za baadhi ya wanachama wa serikali ya Zimbabwe na watu wengine za kudhoofisha mchakato wa kidemokrasia nchini humo bado lipo pale pale. Amesema ni kutokana na sababu hiyo ndio maana ameona kuna umuhimu wa kuendeleza kwa nguvu vikwazo kwa Rais Mugabe na watu wake wa karibu ili wachukue hatua kuhusu suala hilo. Hata hivyo katika upande wa hatua chanya kwa Harare, serikali ya Uingereza imethibitisha kuwa, Mark Lowcock Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa nchi hiyo wiki hii ataelekea Zimbabwe kwa ajili ya mazungumzo na Patrick Chinamasa Waziri wa Fedha na maafisa wengine wa nchi hiyo. Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza amesema kuwa, nchi yake itaendelea kuwasaidia watu maskini wa Zimbabwe na kufanya kila inaloweza ili kuimarisha demokrasia, uthabiti na ustawi katika nchi hiyo. 
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)