TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Umoja wa Afrika kuongeza vikosi vya jeshi dhidi ya Boko Haram

Umoja wa Afrika kuongeza vikosi vya jeshi dhidi ya Boko HaramBaraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika jana lilikubali suala la kuongeza idadi ya vikosi vya jeshi la kieneo kwa ajili ya kupambana na kundi la Boko Haram. Jeshi hilo ambalo Januari mwaka huu Umoja wa Afrika ulikubali liundwe kwa minajili ya kupambana na wanamgambo wa kundi la Boko Haram, linatarajia kuongeza idadi ya wanajeshi wake kutoka 8700 na kufikia 10,000. Wanajeshi hao watatoka Nigeria, Niger, Cameroon, Chad na Benin na makao makuu ya jeshi hilo yatakuwa Nd’jamena mji mkuu wa Chad.
Rais Idriss Derby wa Chad hivi karibuni alisisitiza suala la kuangamizwa kikamilifu kundi la kigaidi la Boko Haram. Baadhi ya wapembuzi wa mambo wameitathmini hatua ya Rais Derby kutuma mapema vikosi vya jeshi katika mpaka wa nchi za Nigeria na Cameroon kuwa ni katika jitihada za kiongozi huyo za kutaka kuwa na nafasi muhimu katika eneo hilo. Serikali ya Nigeria nayo imetoa radiamali kali kuhusu suala la kutumwa wanajeshi wa Chad katika maeneo ya mipaka ya pamoja ya nchi hizo. Radiamali hiyo imetokana na wasiwasi wa serikali ya Nigeria kuhusu uwezekano wa Chad kuwa na ushawaishi na kuingia katika ardhi yake.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Umoja wa Afrika, vikosi hivyo vya muungano wa jeshi la kieneo havitaingia katika ardhi ya Nigeria, bali vitapelekwa katika maeneo yanayolizunguka ziwa Chad.
Wasiwasi wa serikali ya Nigeria kuhusu suala la kutumwa nchini humo vikosi vya kigeni katika kipindi hiki cha kukaribia uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika katika miezi ya Machi na Aprili mwaka huu ni jambo linaloweza kueleweka.
Wataalamu ya masuala ya kiusalama walitahadharisha kuwa, mashambulizi ya kundi la kigaidi la Boko Haram yataongezeka sambamba na kukaribia wakati wa kufanyika uchaguzi nchini Nigeria. Inaonekana kuwa, makubaliano yaliyofikiwa kati ya vyama kumi vya kisiasa kwa ajili ya kuzuia ghasia za uchaguzi, yatapunguza wasiwasi uliojitokeza ndani ya nchi hiyo. Pamoja na hayo yote, wasiwasi kuhusu harakati za kundi la kigaidi la Boko Haram utaendelea kuwapo, iwapo vyanzo vya fedha na silaha zinazohitajika kwa ajili ya kuanza operesheni ya jeshi dhidi ya Boko Haram havitaweza kudhaminiwa. 
Ostia Chidoka ambaye ni mshauri wa Rais Goodluck Jonathan wa Nigeria ametahadharisha kuwa, nchi za Magharibi pia zitakabiliwa na hatari ya kundi la kigaidi la Boko Haram. Kwa mtazamo huo, iwapo jamii ya kimataifa haitaiunga mkono kifedha na kisilaha serikali na jeshi la Nigeria katika operesheni ya kuliangamiza kundi la Boko Haram, mashambulizi ya kundi hilo la kigaidi yatavuka mipaka ya Nigeria na Afrika na kuzitishia nchi za bara Ulaya kama Uingereza. Hatua ya wanamgambo wa Boko Haram ya kuiga vitendo vya ukatili vya kundi la kigaidi la Daesh kama kuwauwa watu kwa kuwakata vichwa, inatia nguvu dhana hiyo.
Weledi wa mambo wanaamini kuwa matamshi ya mshauri wa Rais wa Nigeria yumkini yakawa na ukweli. Pamoja na hayo yumkini tahadhari hiyo ikawa na lengo la kuvutia fikra za waliowengi duniani, ambao macho na masikio yao wameelekezwa kwenye matukio yanayojiri ndani ya Syria na Iraq kuhusiana na jinai na ukatili unaofanywa na kundi la kigaidi la Daesh. Uwezekano mwingine ni kuwa, tahadhari ya Ostia Chidoka ni aina fulani ya kuziomba msaada nchi za Magharibi kama Marekani na Uingereza kwa ajili ya kupambana na Boko Haram.
Goodluck Jonathan, mgombea wa chama tawala katika uchaguzi wa rais wa Nigeria anajua vyema kuwa anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa Muhammadu Buhari. Katika mazingira kama hayo, iwapo jeshi la kieneo litashindwa katika vita vyake dhidi ya Boko Haram, basi suala hilo litachangia kwa kiasi kikubwa kushindwa mgombea wa chama tawala katika uchaguzi huo.

Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)