TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Vyama vya upinzani nchini Sudan kususia uchaguzi mkuu

Vyama vya upinzani nchini Sudan kususia uchaguzi mkuu Vyama kadhaa vya upinzani nchini Sudan vimeamua kususia uchaguzi mkuu ujao wa bunge na rais wa nchi hiyo uliopangwa kufanyika tarehe 13 Aprili. Chama tawala cha Congress ya Taifa kitachuana na vyama vingine zaidi ya 40 katika uchaguzi huo. Kwa mujibu wa Tume Huru ya Uchaguzi ya Sudan. Zaidi ya watazamaji wa kimataifa wapatao 60,000 kutoka nchi za Kiarabu, Umoja wa Afrika na Jumuiya ya IGAD wanatazamiwa kusimamia uchaguzi huo.
Huku ikikosoa hatua ya vyama vya upinzani ya kususia uchaguzi huo, serikali ya Khartoum imesema kuwa viongozi wa vyama hivyo hawafai kuiongoza nchi hiyo. Kwa kuongezeka wimbi la upinzani nchini Sudan inaonekana kuwa hali ya mambo nchini humo itakuwa ngumu zaidi kwa kuzingatia kukaribia kufanyika zeozi la uchaguzi nchini. Awali chama tawala kilikuwa kimekiri kuwepo upinzani kuhusiana na suala zima la uchaguzi na hivyo kuitisha mazungumzo ya kitaifa ili kujaribu kupunguza tofauti zilizopo kuhusu suala hilo. Hii ni katika hali ambayo hadi sasa hakuna hatua yoyote ya maana iliyochukuliwa kwa lengo la kutuliza hali ya mambo nchini, bali kinyume chake serikali imekuwa ikikamata na kuwatia mbaroni viongozi wa upinzani na hivyo kukiuka misingi ya demokrasia na vilevile kuvuraga zaidi hali ya mambo nchini. Ni kutokana na suala hilo ndipo baadhi ya wataalamu wa mambo wakasema kuwa hali hiyo huenda ikaharibu zaidi hali ya mambo nchini Sudan hasa katika kipindi hiki nyeti cha kukaribia uchaguzi mkuu.Wataalamu hao wanasema kuwa mashindano ya uchaguzi kati ya Rais Omar al-Bashir na wapinzani si ya kiadilifu hata kidogo. Katika hali ambayo rais huyo anatumia mali na vyombo vya habari vya umma kwa lengo la kuendeshea kampeni zake za uchaguzi, wapinzani wamenyimwa haki hiyo.
Katika upande wa pili marekebisho yaliyofanyika katika katiba ya Sudan, yanampa Rais Bashir uwezo wa kuwachagua magavana wa majimbo katika hali ambayo magavana hao wanapasa kuchaguliwa moja kwa moja na wananchi. Katika upande wa pili, uchaguzi hautafanyika katika majimbo ya Darfur, Jabal an-Nuba na Blue Nile kutokana na kuendelea mapigano katika majimbo hayo. Kutokuwepo vyombo huru vya mahakama nchini Sudan ni jambo jingine ambalo limezidisha mivutano ya kisiasa nchini humo. Vyombo hivyo kwa sasa vinadhibitiwa kikamilifu na serikali na rais ndiye aliye na uwezo wa kuwapa na kuwafuta kazi majaji wa mahakamu kuu. Wanachama wa tume huru ya uchaguzi pia wanateuliwa moja kwa moja na rais, jambo linalowafanya waogope kumkosoa kwa njia yoyote ile. Wapinzani pia wanasema kuwa Rais Bashir hafai kuiongoza nchi kutoka na kuwa anasakwa na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC. Kushindwa serikali ya al-Bashir kuimarisha uchumi wa Sudan ni sababu nyingine inayotolewa na wapinzani dhidi yake. Hivi sasa viwanda vingi vya nchi hiyo vimefilisika na madeni yake ya nje yanapindukia dola bilioni 40. Wapinzani pia wanaashiria kujitenga Sudan Kusini na Sudan na tetesi za kujitenga maeneo mengine ya nchi hiyo likiwemo jimbo la Darfur, kuwa miongoni mwa mambo yanayowafanya wadai kuwa al-Bashir hana tena uwezo wa kuongoza nchi. Wataalamu wa mambo pia wanaashiria kuenea ufisadi, rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma unaofanywa na viongozi wa ngazi za juu serikalini kuwa baadhi ya mambo ambayo yangemfanya Bashir ashindwe kwenye uchaguzi, kama uchaguzi huo ungekuwa huru na wa haki.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)