TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Kushadidi hukumu za kidhulma nchini Misri

Kushadidi hukumu za kidhulma nchini MisriHabari kutokna nchini Misri zinaonesha kuongezeka mwenendo wa hukumu kali na za kidhulma dhidi ya wapinzani na matukio ya nchi hiyo yanaonesha kuwa, vyombo vya mahakama vya nchi hiyo kivitendo vimegeuzwa na watawala wa Misri na kuwa wenzo wao wa kuwakandamiza wapinzani lengo likiwa ni kunyamazisha sauti yoyote ile ya malalamiko. Kuhusiana na hilo, Rais aliyepinduliwa na jeshi Muhammad Mursi amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela. Mahakama ya Jinai ya Cairo Jumanne ya jana ilimhukumu kifungo cha miaka 20 jela Muhammad Mursi kwa tuhuma za kuchochea machafuko, mauaji na kuwatesa waandamanaji. Hili ni faili la kwanza la kesi miongoni mwa mafaili matano ya kesi zinazomkabili Mursi. Rais huyo wa zamani wa Misri anaweza kukata rufaa kulalamikia hukumu hiyo ya mahakama ya jinai. Hii ni hukumu ya kwanza kutolewa dhidi ya Mursi tangu alipoondolewa madarakani na jeshi tarehe 3 Julai mwaka 2013; na imepangwa kuwa tarehe 16 ya mwezi ujao wa Mei, Mursi atasomewa mashtaka ya mafaili mengine mawili ya kesi zinazomkabili. Ikumbukwe kuwa, Muhammad Mursi alikuwa Rais wa kwanza wa Misri aliyechaguliwa kupitia uchaguzi huru na aliondolewa madarakani mwaka mmoja tu baada ya kuwa madarakani. Hadi sasa mamia ya wafuasi wa Mursi wamehukumiwa adhabu ya kifo ambapo Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, hukumu kama hizo ni za aina yake na hazijawahi kushuhudiwa. Wakati Muhammad Mursi anasota jela  na akiwa anakabiliwa na hukumu kali. Hivi karibuni Hosni Mubarak dikteta wa zamani wa Misri na wanawe walifutiwa tuhuma na mashtaka yote yaliyokuwa yakiwakabili. Hatua ya Rais Abdul Fattah al-Sisi wa Misri ya kumfutia mashtaka Hosni Mubarak na kumhukumu Mursi inalenga kutokomeza mapinduzi ya wananchi wa nchi hiyo. Hii ni katika hali ambayo, ukandamizaji na mipango ya kutaka kuwafuta katika ulingo wa siasa za Misri wanachama wa Ikhwanul Muslimiin nayo imo katika sera za serikali na vyombo vya mahakama vya nchi hiyo. Katika kipindi hiki wanaharakati elfu 22 wa kisiasa wametiwa mbaroni na jeshi na vyombo vya usalama vya Misri na takribani mia mbili kati yao wamehukumiwa adhabu ya kifo. Kushadidi vitendo vya utumiaji mabavu na kutolewa hukumu kali na za kidhulma nchini Misri dhidi ya wapinzani wa kisiasa kumezitia wasiwasi mkubwa fikra za waliowengi ulimwenguni pamoja na asasi za kutetea haki za binadamu. Licha ya yote hayo wafuasi wa Muhammad Mursi wangali wanamtambua jenerali wa kijeshi Abdul Fattah al-Sisi kwamba, ndiye aliyeongoza wa mapinduzi ya kijeshi na ambaye alipuuza matokeo ya uchaguzi wa Rais wa mwaka 2012 na kumuondoa madarakani Muhammad Mursi Rais halali aliyekuwa ameibuka na ushindi kupitia uchaguzi halali na wa wazi. Wanaharakati wa kisiasa nchini Misri wanasisitiza kwamba, uchaguzi uliokuja kufanyika baadaye na kupelekea jenerali al-Sisi kuibuka na ushindi, ulikuwa wa kimaonyesho na kiini macho cha kuhalalisha mapinduzi ya kijeshi dhidi ya Mursi.  Wachambuzi wa mambo wanaamini kuwa, kuendelea malalamiko ya wananchi wa Misri ambako kunahesabiwa kuwa ni mtihani wa kupima azma na irada ya fikra za waliowengi ulimwenguni mkabala na wanajeshi wa nchi hiyo kunaweka wazi suala hili kwamba, viongozi wa sasa wa Misri wanatoa hukumu kali na za kidhulma ili kuleta wasiwasi na woga na wakati huo huo kujaribu kuhalalisha suala la kumuondoa madarakani Muhammad Mursi.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)