TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Wapinzani Kongo: Hatushiriki uchaguzi wa mabaraza

Wapinzani Kongo: Hatushiriki uchaguzi wa mabarazaMuungano wa vyama vya upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo umetangaza kuwa hautashiriki kwenye uchaguzi wa mabaraza ya mikoa. Vyama 67 vya upinzani nchini Kongo vimetangaza kuwa havitawaarifisha wagombea wao katika uchaguzi huo, iwapo tume huru ya uchaguzi ya nchi hiyo haitatangaza orodha ya uchaguzi wa mabaraza ya mikoa kabla ya kufanyika uchaguzi. Vyama hivyo 67 vya upinzani huko Kongo ambavyo vitatu kati yake vina wabunge katika bunge la taifa la nchi hiyo, vimetaka kukutana na kufanya mazungumzo na maafisa wa tume huru ya uchaguzi ya nchi hiyo ili kujadili suala hilo. Uchaguzi wa mabaraza ya mikoa huko Kongo DR umepangwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu, huku vyama vikiwa na fursa ya kuwaarifisha wagombea wao hadi kufikia mwezi Mei mwaka huu. L'abbe Malu Malu Mkuu wa Tume Huru ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amesema kuwa katika kipindi cha mwaka huu wa 2015 na 2016, chaguzi saba zitafanyika nchini, ambapo uchaguzi wa kwanza utakuwa ni wa mabaraza ya mikoa na wa mwisho utakuwa wa Rais ambao utafanyika mwishoni mwa mwaka kesho wa 2016.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)