
Muungano wa vyama vya upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo 
umetangaza kuwa hautashiriki kwenye uchaguzi wa mabaraza ya mikoa. Vyama
 67 vya upinzani nchini Kongo vimetangaza kuwa havitawaarifisha wagombea
 wao katika uchaguzi huo, iwapo tume huru ya uchaguzi ya nchi hiyo 
haitatangaza orodha ya uchaguzi wa mabaraza ya mikoa kabla ya kufanyika 
uchaguzi. Vyama hivyo 67 vya upinzani huko Kongo ambavyo vitatu kati 
yake vina wabunge katika bunge la taifa la nchi hiyo, vimetaka kukutana 
na kufanya mazungumzo na maafisa wa tume huru ya uchaguzi ya nchi hiyo 
ili kujadili suala hilo. Uchaguzi wa mabaraza ya mikoa huko Kongo DR 
umepangwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu, huku vyama vikiwa na fursa 
ya kuwaarifisha wagombea wao hadi kufikia mwezi Mei mwaka huu. L'abbe 
Malu Malu Mkuu wa Tume Huru ya Uchaguzi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya 
Kongo amesema kuwa katika kipindi cha mwaka huu wa 2015 na 2016, chaguzi
 saba zitafanyika nchini, ambapo uchaguzi wa kwanza utakuwa ni wa 
mabaraza ya mikoa na wa mwisho utakuwa wa Rais ambao utafanyika mwishoni
 mwa mwaka kesho wa 2016.
 
                            About 
                            NELSON PASCHAL KAMUGISHA
 
                            This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
                          
 
 
 
0 comments:
Post a Comment