Real Madrid watampa David
De Gea, 24, pauni milioni 24 kama ada ya usajili, iwapo atamalizia
mkataba wake ulosalia wa mwaka mmoja Old Trafford, wakati atakapoondoka
bure msimu ujao (Daily Mirror), Manchester City wanakaribia kukamilisha
usajili wa pauni milioni 28.5 wa beki wa Valencia Nicolas Otamendi, 27,
huku Eliaquim Mangala, 24, akitarajiwa kwenda Spain kwa mkopo (Daily
Mail), Manchester City wataongeza dau lao la pauni milioni 43 kumtaka kiungo wa Wolfsburg, Kevin De Bruyne (Sky Sports), Tottenham
wapo tayari wiki hii kutoa dau la pauni milioni 15 kumtaka mshambuliaji
wa West Brom, Saido Berahino, 22, huku beki Joleon Lescott, 33, kiungo
Stephane Ssesegnon, 31, Brown Ideye, 26 na Victor Anichebe pia
wakiruhusiwa kuondoka (Telegraph), dau la pauni milioni 5 kutoka Chelsea
kumtaka beki wa Galatasaray Alex Telles limekataliwa (Daily Star),
Everton watamnyatia beki wa Swansea Ashley Williams, 30, iwapo John
Stones, 21, atakwenda Chelsea (Daily Star), meneja wa Everton Roberto
Martinez pia anataka kumsajili mshambuliaji wa Dynamo Kiev Andriy
Yarmolenko (Liverpool Echo), meneja wa West Ham Slaven Bilic anamtaka
kipa wa QPR Robert Green, 35, akitaka kuimarisha makipa wake (Sun),
Newcastle na Everton wanamtaka beki Jannik Vestegaard, 23, wa Werder
Bremen, lakini beki huyo anasema hana habari (Daily Express). . Na
KWINGINEKO KATIKA SOKA
"Sikuwahi kutaka kuondoka" asema Ramos
Beki wa Real Madrid Sergio Ramos amesema hakuwahi kutaka kuondoka Bernabeu, licha ya taarifa kadhaa kumhusisha na kuhamia Manchester United. Ramos, ambaye amesaini mkataba wa miaka mitano amesema: "Wazo langu lilikuwa kubakia hapa na kustaafu hapa kama rais angeruhusu hilo, na na ninashukuru sasa nina changamoto mpya ya kuwa nahodha wa timu hii.
"Sikuwahi kusema nataka kuondoka, nilikuwa kimya. Sikusema chochote kutokana na kuheshimu wachezaji wenzangu na rais, sikuwahi kupiga simu kwenye ofisi yetu na kutaka fedha zaidi."

Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa
KWINGINEKO KATIKA SOKA
"Sikuwahi kutaka kuondoka" asema Ramos
Beki wa Real Madrid Sergio Ramos amesema hakuwahi kutaka kuondoka Bernabeu, licha ya taarifa kadhaa kumhusisha na kuhamia Manchester United. Ramos, ambaye amesaini mkataba wa miaka mitano amesema: "Wazo langu lilikuwa kubakia hapa na kustaafu hapa kama rais angeruhusu hilo, na na ninashukuru sasa nina changamoto mpya ya kuwa nahodha wa timu hii.
"Sikuwahi kusema nataka kuondoka, nilikuwa kimya. Sikusema chochote kutokana na kuheshimu wachezaji wenzangu na rais, sikuwahi kupiga simu kwenye ofisi yetu na kutaka fedha zaidi."
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa
0 comments:
Post a Comment