TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Al Bashir: Nisiposhinda uchaguzi, nitaacha siasa

http://static.guim.co.uk/sys-images/Guardian/Pix/pictures/2008/07/11/omar.jpgRais Omar al-Bashir wa Sudan amesema kuwa, endapo hatashinda katika uchaguzi mkuu ujao nchini humo, basi ataondoka bila ya matatizo katika ulingo wa kisiasa. Al-Bashir aliyasema hayo jana na kuongeza kuwa, kura za Wasudan ndizo zitakazoamua ima aendelee na siasa au la. Rais huyo wa Sudan ameyasema hayo katika hali ambayo ana uhakika wa kushinda uchaguzi huo ujao huku weledi wa mambo wakiyataja matamshi hayo kuwa ya kuwabeza wapinzani wake. Akizungumza mbele ya wafuasi wake katika eneo la Wad Madani lililoko katika jimbo la Jazirah alisisitiza kuwa, wananchi wa Sudan ndio wenye uwezo wa kuamua nani anayestahiki kuongoza taifa hilo. Rais Omar al-Bashir mwenye umri wa miaka 71 amewakosoa vikali wapinzani wake waliotangaza tangu mapema kususia uchaguzi ujao. Uchaguzi wa rais nchini humo umepengwa kufanyika tarehe 13 Aprili mwaka huu. Hii ni katika hali ambayo vyama vingi vya kisiasa na mashirika kadhaa nchini Sudan, yametangaza kumuunga mkono rais huyo, suala linalompa uhakika wa kushinda katika uchaguzi ujao.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)