TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Berlin yaonywa kuhusu sera yake ya uuzaji silaha

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj-f6J2ZU0hA9nh5t69IW5sqVz7VSmp43wCuZGq2CpOWAhP5b4hNI3_Tf_huhTelIcTJ_l3NHJHwVz93n5rA61OaA3l8BrZ9hq2hqy112ubP60VxqsdDaMgXc6Dkgnd7rZelnPDdJQ_U74n/s1600/uss_truman_and_usns_spica.jpg

http://kiswahili.irib.ir/media/k2/items/cache/0fd60787ca1e55e87a75f25c445b1e98_XL.jpg Wanaharakati wa haki za binadamu wa muungano wa Ujerumani wa kupiga vita utumiaji wa watoto kama askari umeitaka Berlin kuzuia silaha kuangukia mikononi mwa watoto wanaotumiwa katika mizozo ya kivita kama wapiganaji. Wanaharakati hao wamewasilisha ombi hilo kwa serikali ya Berlin katika hafla iliyofanyika chini ya anwani "Red Hand Day" kwa lengo la kutiliwa maanani nafasi ya Ujerumani nchi ya tatu muuzaji wa silaha duniani na kushadidi wasiwasi juu ya kutumiwa watoto kama askari jeshi katika mizozo ya kivita. Antje Weber kutoka Muungano huo unaoendesha mapambano ya kupiga vita utumiaji wa watoto vitani amesema kuwa baadhi ya nyakati, Ujerumani inaiuzia silaha Saudi Arabia, ambapo Saudia pia huzituma silaha hizo katika maeneo yenye mizozo kama Syria ambako silaha hizo hutumika na wakati mwingine hutumbukia mikononi mwa watoto. Inafaa kuashiria hapa kuwa, Ujerumani huuza silaha na zana za kijeshi katika nchi kama Pakistan, India, Misri, Kuwait na Colombia. Ripoti ya hivi karibuni ya Umoja wa Mataifa inaeleza kuwa, nchi hizo zina makundi yanayobeba silaha yanayowatumia watoto kama askari. Ujerumani pia ni moja ya nchi kubwa zinazounda silaha ndogo ndogo ambazo zinaweza kubebwa na watoto wadogo kiurahisi. 
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)