TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Harakati ya al Houthi haitosalimu amri mbele ya vitisho

Mohammed Abdul-Salam msemaji wa harakati ya al Houthi ya nchini Yemen Mohammed Abdul-Salam msemaji wa harakati ya al Houthi ya nchini YemenHarakati ya Kiislamu ya al Houthi ya nchini Yemen imesema kuwa, haitosalimu amri mbele ya vitisho kufuatia wito uliotolewa na nchi jirani kuutaka Umoja wa Mataifa kutumia nguvu kuhusiana na hali ya usalama ya nchi hiyo.
Mohammed Abdul-Salam msemaji wa harakati ya al Houthi ya nchini Yemen amesema kuwa watu wa nchi hiyo hawataachana na mapinduzi yao kwa kuogopa vitisho.
Ameyasema hayo leo ikiwa ni siku moja baada ya Mawaziri wa Mambo ya Nje wa nchi sita wanachama wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi kuliomba Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuingilia kijeshi huko Yemen.
Siku kadhaa zilizopita nchi zisizopungua tisa zimefunga balozi zake na kuwaondoa wanadiplomasia wake huko Yemen kwa madai ya kuzorota kwa hali ya usalama nchini humo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)