TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Kabila apinga uingiliaji wa kimataifa dhidi ya waasi

Kabila apinga uingiliaji wa kimataifa dhidi ya waasi Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo amekosoa vikali uingiliaji kati wa kimataifa katika masuala ya nchi hiyo. Rais Joseph Kabila amepinga vikali pendekezo la uungaji mkono wa kijeshi wa Umoja wa Mataifa dhidi ya waasi wa Kihutu wa FDLR wa nchini Rwanda walioko mashariki mwa nchi hiyo. Matamshi ya Rais Kabila yanatolewa katika hali ambayo, siku chache zilizopita,  Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa MONUSCO kilitangaza kusitisha utekelezaji wa operesheni ya pamoja na jeshi la Kongo kwa lengo la kuliangamiza kundi la waasi wa FDLR, baada ya umoja huo kuwatuhumu majenerali wawili wa jeshi la Kongo kwa vitendo vya ukiukaji wa haki za binadamu. Rais Kabila amewaeleza wanadiplomasia walioko mjini Kinshasa kwamba, jeshi la Kongo limeshaanza kutekeleza operesheni ya kijeshi dhidi ya waasi wa FDLR huko mashariki mwa Kongo bila ya msaada wowote wa vikosi vya MONUSCO. Umoja wa Mataifa umeeleza kuwa, kuna waasi wa Kihutu wapatao 1,400  katika eneo la Ukanda wa Maziwa Makuu ya Afrika kwa muda wa miaka ishirini sasa.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)