TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Wapinzani DRC waikosoa Tume ya Taifa ya Uchaguzi

Wapinzani  DRC waikosoa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Vyama vya upinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo vimeeleza kuwa , Tume ya Taifa ya Uchaguzi imewahadaa wananchi baada ya kukurupuka na kutangaza tarehe ya uchaguzi wa rais nchini humo. Taarifa iliyotolewa na wapinzani nchini Kongo vimeeleza kuwa, Tume ya Taifa ya Uchaguzi imetangaza tarehe ya kufanyika uchaguzi wa rais bila ya kuzingatia uhalisia wa mambo. Taarifa hiyo imeeleza kuwa, vyama vya upinzani haviwezi kuipinga tarehe iliyoainishwa kufanyika uchaguzi huo, bali imeeleza kwamba uamuzi huo wa tume umefanyika bila ya kuwashirikisha viongozi, wanasiasa na wawakilishi kutoka makundi ya kijamii na kiraia. Hivi karibuni, Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Kongo ilitangaza kwamba, uchaguzi wa rais nchini humo utafanyika tarehe 27 Novemba mwakani. Tume ya Uchaguzi ya Kongo ilitangaza kuwa uchaguzi wa bunge nao utafanyika tarehe hiyohiyo. Hapo awali, serikali ya Kinshasa ilifanya juhudi za kutaka kuakhirisha uchaguzi wa rais hadi mwaka 2018, suala ambalo lililalamikiwa na kupingwa vikali na vyama vya upinzani na makundi ya kiraia nchini humo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)