TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Zuma awasilisha mpango wa marekebisho ya ardhi

Zuma awasilisha mpango wa marekebisho ya ardhi Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ameandaa muswada wa kuuwasilisha bungeni wenye lengo la  kufanyiwa  marekebisho ya kimsingi sheria ya kumiliki ardhi nchini humo. Taarifa kutoka Pretoria zinasema kuwa, mpango huo wa Rais Zuma utawazuia raia wa kigeni kumiliki ardhi nchini humo. Kwa mujibu wa mpango huo, wazalendo wa Afrika Kusini wataweza kumiliki ardhi isiyozidi ukubwa wa hekta elfu kumi na mbili na wageni wote hawataruhusiwa kumiliki ardhi, bali watakodishwa kwa muda wa kati ya miaka 30 hadi 50. Hatua ya Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ina mwelekeo wa kupata uungaji mkono kutoka kwa wazalendo wausi walio wengi nchini humo, na hasa ikizingatiwa kuwa utajiri mkubwa wa nchi hiyo unamilikiwa na wageni. Nchi za Kiafrika zinakabiliwa na migogoro mingi ya umiliki wa ardhi, kutokana na matajiri na wageni kujilimbikizia maeneo makubwa ya ardhi huku wenyeji wakiambulia sehemu ndogo tu ya ardhi zisizo na rutuba kwa  shughuli za kilimo na ufugaji. Inafaa kuashiria hapa kuwa, miaka ya hivi karibuni Zimbabwe ilitumbukia kwenye mgogoro mkubwa na nchi za magharibi, baada ya Rais Robert Mugabe wa nchi hiyo kuwanyang'anya wageni mashamba makubwa waliyokuwa wakiyamiliki na badala yake kuwapatia maveterani wa vita na wazalendo wa nchi hiyo, suala lililokabiliwa na upinzani mkubwa kutoka nchi za Magharibi.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)