TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

LEO KATIKA HISTORIA Jumapili, 3 Jamadul-Awwal 1436 Hijria

Jumapili, 3 Jamadul-Awwal 1436 Hijria Leo ni Ijumapili tarehe 3 Jamadul-Awwal 1436 Hijria, inayosadifiana na tarehe 22 Februari  mwaka 2015 Miladia.  
Siku kama ya leo miaka 9 iliyopita, inayosadifiana na 22 Februari 2006, Haram mbili takatifu za Maimamu al Hadi na Hassan al-Askari katika mji wa Samarra nchini Iraq, ziliharibiwa vibaya kwenye mashambulizi kadhaa ya miripuko ya mabomu yaliyofanywa na makundi ya kigaidi na kupelekea hasara kubwa za mali na watu. Maimamu hao ni wajukuu wa Mtume Bwana Mtume Muhammad SAW, na waliokuwa na nafasi kubwa ya kielimu na uchaji-Mungu katika zama zao. Kitendo cha kuharibiwa eneo hilo kiliwakasirisha mno Waislamu duniani hususan wafuasi wa Ahlul Bait wa Mtume (saw). Nukta ya kufaa kukumbusha ni kwamba, kabla ya kujiri mashambulizi hayo, ulinzi wa haramu hizo, ulikuwa kwa majeshi vamizi ya Marekani. Shambulio hilo lilifanyika kwa lengo la kuzusha ufa kati ya safu za Waislamu wa madhehebu za Shia na Suni nchini Iraq.
Siku kama ya leo miaka 57 iliyopita, inayosadifiana na 22 Februari 1958, Abul-Kalaam Ahmad Azad, msomi, khatibu na mwanasiasa wa India alifariki dunia akiwa na umri wa miaka 70. Abul Kalaam Azad alinza harakati za kisiasa akiwa na umri wa miaka 17 dhidi ya utawala wa kikoloni wa Uingereza kwa shabaha ya kuwazindua Waislamu wa India. Msomi huyo aliwekwa gerezani mara kadhaa na wakoloni kutokana na hatua zake za kuchapisha na kutoa hotuba zenye kufichua ukandamizaji wa Uingereza. Baada ya India kuwa huru, alichaguliwa kuwa mbunge na Waziri wa Elimu wa nchi hiyo.
Siku kama ya leo miaka 97 iliyopita, Mirza Swadiq Hakim, maarufu kwa jina la Adibul-Mamaalik Farahani, alifariki dunia. Akiwa kijana mdogo, Mirza alisoma elimu mbalimbali na fasaha ya lugha ya Kifarsi na lugha nyengine za Ulaya. Kwa miaka yote Adibul-Mamaalik, alijishughulisha na uandishi sanjari na kusimamia idara za magazeti ya lugha na shughuli nyengine za kiserikali. Mbali na hayo msomi huyo alitabahari pia katika uwanja wa mashairi kwa kufuata nyendo za watalamu wa zamani wa mashairi.
Na siku kama ya leo, miaka 144 iliyopita, alifariki dunia Ayatullah Mirza Abu Abdillah, Sheikhul-Islami Zanjani, msomi mkubwa na mshairi wa Kiislamu. Msomi huyo mkubwa, alizaliwa mwaka 1224 Hijiria mjini Zanjani, moja ya miji ya Iran na kuelekea mjini Isfahani kwa ajili ya masomo akiwa kijana mdogo. Akiwa Isfaham Ayatullah Mirza Abu Abdillah alipata kusoma katika hauza ya kielimu ambayo ilikuwa na itibari kubwa kielimu wakati huo. Baada ya kuhitimu masomo yake alirejea eneo alikozaliwa na kujishughulisha na kuwalea wanafanzu wake.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)