TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Tanzania,Namibia,Uganda zashinda michuano ya kriketi



 Baada ya kuanza vibaya kwa kufungwa na Namibia kwa mikimbio 102, wenyeji Tanzania wamefanikiwa kuuona mwezi baada ya kuwafunga Botswana kwa mikimbio (runs) 47) katika michuano ya Afrika kwa wavulana chini ya miaka 19 ya kriketi kwa ajili ya kufuzu kucheza kombe la Dunia inayoendelea Dar es Salaam.
Tanzania walishinda tosi na kuanza mchezo kwa kupata mikimbio 174 (all out) katika ova 44.4 katika inning (zamu) yao huku Botswana wakishindwa kufikia mikimbio hiyo na kupata runs 127 ( wachezaji wote wakitolewa-allout) katika ova 46.5.
Kocha wa Tanzania, Khali Rehemtulla amesema licha ya kupoteza mechi ya ufunguzi mwishoni mwa wiki, ana mategemeo ya kuwa mabingwa na kufuzu kucheza kombe la Dunia mwakani huko Dhaka, Bangladesh.
Namibia wameendeleza ushindi kwa kuwafunga Nigeria kwa runs 164 wakati Kenya ilifungwa na Uganda kwa runs 26 katika mchezo mkali uliofanyika klabu ya Gymkhana.
Uganda walifanikiwa kupata runs 95/10 (all out) wakati Kenya walipata runs 69/10 ( all out).
Huo ni ushindi wa pili kwa Uganda, baada ya siku ya ufunguzi kuwafunga Botswana kwa wiketi saba.
Licha ya huzuni ya kufungwa na Uganda Jumapili, Kenya walikuwa na furaha mwishoni mwa wiki kwa kuwafunga Nigeria kwa wiketi saba pia katika mechi ya ufunguzi.
Michuano hiyo inaendelea kwa mechi kadhaa kuchezwa.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)