TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Thailand yakataza mimba za biashara

Sheria inayowakataza wapenzi wawili wa kigeni wanaotaka kushika mimba kupitia mtu mwengine kwa njia ya malipo imeanza kutekelezwa nchini Thailand.
Sheria hiyo ilibuniwa baada ya wanawake kadhaa nchini Thailand kubeba mimba ya wateja wao wa kigeni.


Kumeshuhudiwa kashfa kadhaa za ubebaji mimba miongoni mwa wateja wa nje ya nchi, ikiwemo kesi maarufu ya wapenzi wawili wa Australia waliomuacha mwana wao wa kiume na mamake aliyemzaa kwa sababu aliyezaliwa na ulemavu, lakini wakamchukua dadake pacha aliyezaliwa bila ya matatizo yote na kumhamisha hadi Australia.
Sheria hiyo mpya haipigi marufuku malipo yote ya ubebaji mimba kwa niaba ya mteja wa kigeni, lakini inafanya kinyume cha sheria matumizi ya mawakala au kupigia debe matangazo ya wanawake wanaotaka kuwabebea wengine watoto.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)