TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Maandamano ya amani ya wanadini yafanyika UK

Maandamano ya amani ya wanadini yafanyika UK Viongozi wa madhehebu za dini mbalimbali nchini Uingereza wamefanya maandamano katika mitaa ya katikati mwa jiji la London lengo kuu likiwa ni kuimarisha kuishi kwa upendo na amani kati ya wafuasi wa dini mbalimbali. Viongozi na shakhsia wa madhehebu mbalimbali za Kiislamu, Kikristo na Kiyahudi wa nchini Uingereza wameshiriki kwenye maandamano hayo yaliyohudhuriwa na watu zaidi ya mia moja huko London.
 Washiriki wa maandamano hayo wamesisitiza sualal la kuwepo amani na maelewano kati ya wafuasi wa dini mbalimbali na kupinga hatua zenye kuchochea chuki za kidini na vitendo vya ukatili kwa jina la dini vinavyojiri katika maeneo mbalimbali. Mwakilishi wa Waislamu katika maandamano hayo ya London amesisitiza kuwa wafuasi wa dini mbalimbali wanataka amani, kuishi kwa maelewano na kuheshimiana kila mmoja. Maandamano ya amani ya mjini London ambayo ni jibu kwa mashambulizi ya hivi karibuni katika miji ya Paris na Copenhagen, yameandaliwa na kundi la viongozi wa kidini wa Uingereza chini ya anuani" mpango wa kuishi kwa amani kati ya wafuasi wa dini mbalimbali."
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)