TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Tutawakimbiza

http://static.goal.com/770000/770032_gallery.jpg
 KOCHA wa Yanga, Hans Pluijm, ametamka kwamba amepata karibu kila kitu kuhusu wapinzani wao wa Kombe la Shirikisho, BDF XI ya Botswana na hapohapo akatamka staili moja muhimu watakayoitumia kuwaumiza wanajeshi hao kuwa ni kasi ya kutosha kwa viungo wake.
Akizungumza na Mwanaspoti, Pluijm alisema amepata marafiki zake wengi kutoka Afrika Kusini ambao wamemsaidia kupata mbinu za kuwaumiza BDF XI kwa kumpatia mkanda mmoja wa video ya mechi za timu hiyo ambao wamemtaka kutumia viungo wenye kasi kuwachosha wanajeshi hao.
Katika kujipanga na hilo, Pluijm ameanza mikakati ya kuwapa kazi viungo; Simon Msuva, Mrisho Ngassa na Andrey Coutinho kuwachosha BDF XI kwa kufungua uwanja.
Pluijm alisema kasi ndiyo silaha pekee ambayo itawasaidia kuwaumiza wapinzani wao hao ambao zaidi ametahadharishwa kwamba wanajeshi hao wapo vizuri kwa fiziki ingawa mabadiliko ya hali ya hewa yanaweza kuwaathiri.
Alisema Botswana haina tofauti kubwa na Afrika Kusini ambao wamekuwa na hali ya hewa ya baridi na hivyo watapata tabu kidogo kutokana na joto la Dar es Salaam.
“Nimepata kila kitu, kwa sasa la muhimu ni kuangalia maandalizi yetu, naweza kusema tupo tayari kwa vita na hao wanajeshi,” alisema Pluijm.
“Nimeambiwa kwamba tunatakiwa kutumia kasi kuwaumiza hawa jamaa na hilo hatuna shaka nalo kwa kuwa watu wa kutufanyia kazi hiyo tunao katika timu yetu, mtu kama Simon (Msuva) na Ngassa (Mrisho) ni watu mwafaka kwa hilo.”
Yanga itaumana na BDF kesho Jumamosi Uwanja wa Taifa Dar es Salaam.
CANNAVARO
Katika hatua nyingine, Pluijm ametamka kwamba licha ya matarajio makubwa aliyonayo nahodha wake Nadir Haroub ‘Cannavaro’ ndiye mtu pekee anayemchanganya.
Pluijm alisema Cannavaro amezua hofu katika kambi yao kufuatia kupata maumivu ya goti la kulia ambapo bado haijajulikana juu ya majaliwa yake.
Pluijm alisema Cannavaro atalazimika kusubiri kwa siku mbili kuanzia jana kujua hatma yake kama atakuwa tayari kwa mchezo huo wa kwanza baina ya timu hizo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)