TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

UN yawalaani mashabiki wa Chelsea kwa kumbagua Mfaransa Mwafrika

UN yawalaani mashabiki wa Chelsea kwa  kumbagua Mfaransa Mwafrika Ofisi ya haki za Binadamu katika Umoja wa Mataifa, imelaani vikali vitendo vya ubaguzi wa rangi vilivyofanywa na mashabiki wa kandanda kutoka klabu ya Uingereza ya Chelsea, wakati klabu hiyo ikijiandaa kushiriki michuano ya Ligi ya Mabingwa wa Ulaya mjini Paris Jumanne iliyopita. Mashabiki hao wa Chelsea walinaswa kwenye kamera wakiimba nyimbo za kujigamba kwa ubaguzi wao wa rangi, huku wakimzuia raia mmoja wa Ufaransa mwenye asili ya Afrika kupanda kwenye treni kwa kumsukuma nje. Ofisi ya Haki za Binadamu imesema katika miaka ya hivi karibuni, imekuwa ikifanya mashauriano na Shirikisho la Soka Duniani, FIFA na Shirika la Soka Ulaya, UEFA kuhusu kutafuta njia za kuendeleza juhudi za kutokomeza ubaguzi wa rangi katika mchezo wa kandanda baada ya matukio mengi ya vitendo vya kibaguzi, hususan ndani ya viwanja vya mpira. Rupert Colville ni msemaji wa Ofisi ya haki za binadamu amesema: "Hili siyo tukio moja tu, vitendo kama hivi vya kikatili na ubaguzi wa rangi hutokea kila siku barani Ulaya lakini haviibui hasira kiasi hicho kwa kuwa havinaswi kwenye kamera." Amesema vitendo vya stesheni ya treni ya Richelieu-Drouot mjini Paris vimeonyesha kuwa bado kuna kazi nyingi ya kufanya kabla ya kutokomeza ubaguzi wa rangi katika soka na katika jamii kwa ujumla.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)