TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Vyama vya siasa TZ vitangulize maslahi ya wananchi

http://www.thehabari.com/wp-content/uploads/2014/03/warioba.jpgWaziri Mkuu mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Joseph Warioba amevitaka vyama vya siasa nchini humo kuzingatia matakwa ya wananchi katika suala zima la Kura ya Maoni ya Katiba Inayopendekezwa badala ya kuwagawa. Warioba amesema anaamini kwamba, baadhi ya vipengele vilivyokataliwa katika Rasimu ya Katiba, ipo siku vitafanyiwa kazi kuondoa migongano huku akisisitiza, kisheria kura ya maoni siyo mwisho wa mchakato. Waziri Mkuu huyo mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema kuwa, kwa sasa, badala ya kuwaweka wananchi pamoja na kukubaliana wanachotaka , upo mvutano huku wengine wakitaka Katiba Iliyopendekezwa ikubaliwe na wengine wakitaka wananchi waikatae. Hayo yanajiri katika hali ambayo mrengo wa upinzani nchini Tanzania chini ya mwavuli wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) umetangaza kutoshiriki katika kura ijayo ya maoni ya Katiba. Aidha akihutubia mkutano wa hadhara hivi karibuni huko Zanzibar, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) Maalim Seif Sharif Hamad alitangaza rasmi kwamba, chama chake hakitashiriki katika kura hiyo ya maoni ya Katiba iliyopendekezwa kutokana na kupuuzwa matakwa ya wananchi.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)