TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Wazalishaji, wasambazaji waaswa kuingiza Sukari sokoni

Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika imewaagiza wazalishaji na wasambazaji wakubwa wa sukari nchini kuingiza Sukari sokoni na kuhakikisha inapatikana kwa bei ambayo watanzania wanaweza kuimudu.

Maagizo hayo yametolewa baada ya Serikali kuzuia sukari ya nje kuuzwa hapa nchini hali iliyosababisha kupanda kwa bei ya sukari kati ya shilingi 2500 hadi 3000.


http://startvtz.com/wp-content/uploads/2015/02/wassira-steven-100x100.jpgAkizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika Steven Wasira amesema miezi miwili iliyopita wazalishaji na wasambazaji wa sukari walisema hawawezi kuwekeza kutokana na soko la sukari nchini kuharibiwa na sukari inayotoka nje kitendo kilichoilazimu Serikali kutaka kujua njia zinazoingiza sukari hiyo.

Amesema baada ya Serikali kuchukua hatua za kuziba mianya ya uingizwaji wa sukari bila kodi na kudhibiti sukari inayopita nchini isibaki isafirishwe kwa kujua kuwa sukari inayozalishwa nchini inatosha, ndipo tatizo la uhaba wa sukari likaibuka na kusababisha bei kupanda, na Serikali ikaona haja ya kukutana na wazalishaji na wasambazaji na kufanya makubaliano

Amesema Sukari iliyopo nchini ni tani elfu 40  na endapo itaingizwa sokoni na kuuzwa bila matatizo yoyote Serikali itawapa vibali wafanyabiashara hao kuagiza tani laki 1 za sukari nje ili kufidia kipindi ambacho viwanda hufungwa kwa ajili ya matengenezo kuanzia mwezi April mpaka mwezi Mei ambapo hufunguliwa na kuendelea kuzalisha kama kawaida.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)