TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Indhari ya IMF kuhusiana na hali ya kiuchumi nchini Zimbabwe

Indhari ya IMF kuhusiana na hali ya kiuchumi nchini ZimbabweWataalamu wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa IMF wamesema kuwa, Zimbabwe itakabiliwa na hali mbaya ya kiuchumi katika mwaka huu wa 2015. Kwa kuzingatia ukuaji duni wa kiuchumi nchini Zimbabwe sambamba na madeni mengi yanayoikaba koo nchi hiyo, basi yamkini nchi hiyo ya kusini mwa Afrika ikakabiliwa na matatizo mengi. Domenico Fanizza, Mkuu wa Kamati ya Mfuko wa Fedha wa Kimataifa IMF iliyotumwa Harare Zimbabwe amesema hayo katika safari yake nchini humo. Lengo la safari hiyo limetajwa kuwa ni kuchunguza ukuaji wa uchumi pamoja na uwazi kuhusiana na kiwango cha madeni ya nchi hiyo. Licha ya kushuka bei ya mafuta katika soko la dunia, wataalamu wa mambo wanatabiri kwamba, uchumi wa Zimbabwe utazidi kulegalega mwaka huu. Ni karibu muongo mmoja sasa ambapo uchumi wa Zimbabwe umedorora kutokana na kiwango cha juu cha ukosefu wa ajira na ukuaji wa kusuasua wa uchumi wa nchi hiyo. Baadhi ya wachambuzi wa mambo wanaamini kuwa, sera mbovu za kiuchumi za serikali ya Harare katika miongo ya hivi karibuni ndizo zilizoufanya uchumi wa nchi hiyo kukabiliwa na hali mbaya. Rais Robert Mugabe mwaka 2000 alianza kutekeleza mpango wa marekebisho ya ardhi katika maeneo yote ya nchi hiyo. Lengo la mpango huo lilikuwa ni kupora ardhi bora kwa kilimo za wazungu na kuzigawa baina ya wazalendo masikini wa nchi hiyo. Sera za Rais Mugabe za kukabiliana na wakoloni wa zamani wa Ulaya kama Uingereza zimemfanya aendelee kubakia madarakani kutokana na himaya na uungaji mkono wa wazalendo weusi wa nchi hiyo katika kila chaguzi. Sera hizo za Mugabe zimekuwa zikiwavutia wapiga kura wazalendo weusi ambao ndio wanaounda asilimia kubwa ya wakazi wa nchi hiyo ya kusini mwa Afrika. Pamoja na hayo, utumiaji mabavu wa wafuasi wenye misimamo mikali wa chama tawala cha ZANU-PF katika kupora ardhi na kuwauwa wamiliki weupe wa ardhi kuliitumbukiza nchi hiyo katika mgogoro ambapo hadi sasa athari mbaya za mgogoro huo zingali zinashuhudiwa. Katika upande mwinginme, kufukuzwa wazungu elfu nne katika ardhi walizokuwa wakizimikili na kisha ardhi hizo kugawia wazalendo weusi wa nchi hiyo, kulipelekea wazungu wengi waliowachache kuikimbia nchi hiyo. Kutokuwa na tajiriba wazalendo weusi wa Zimbabwe katika masuala ya kilimo na kukosa vyanzo vya fedha kuliifanya sekta ya kilimo Zimbabwe idorore katika kipindi cha muda mfupi. Kuadimika bidhaa za mazao kama mahindi nchini Zimbabwe, nchi ambayo katika kipindi fulani ilikuwa mashuhuri kwa jina la “Kikapu cha Mkate Afrika” kwa maaana ya mzalishaji mkubwa wa chakula barani Afrika kuliufanya uchumi wa nchi hiyo uzidi kudidimia. Hata kama Rais Mugabe na viongozi wa chama tawala cha ZANU-PF hawakuwa tayari kukiri kushindwa mpango wa marekebisho wa ardhi, lakini hatimaye tarehe 27 Februari mwaka huu, kiongozi huyo wa Zimbabwe alikiri kwamba, sera za ardhi hazikuwa sahihi. Pamoja na hayo, juma lililopita, Rais Mugabe aliwaonya wakulima weupe kwamba, atawapokonya ardhi wanazomiliki. Weledi wa masuala ya kiuchumi wanaamini kuwa, kukabidhiwa mashamba wazalendo weusi wa Zimbabwe ambao hawakuwa na ustadi katika masuala ya kilimo kulitoa pigo kubwa kwa sekta ya uchumi wa nchi hiyo.

Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)