TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

UM: Tanzania, Malawi na Burundi ziwalinde Albino

UM: Tanzania, Malawi na Burundi ziwalinde Albino Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Zeid Ra'ad Al Hussein, ameelezea wasiwasi wake juu ya ongezeko la mashambulizi dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi, Albino.
Amesema katika kipindi cha miezi sita watu 15 nchini Tanzania, Malawi na Burundi wametekwa na kujeruhiwa na wengine kuuawa akisema watu watatu kati yao wamekumbwa na visa hivyo wiki iliyopita pekee. Kamishna Zeid amesema mashambulio hayo mara nyingi hulenga watoto na matokeo yake Albino wanaishi maisha ya woga ikiwa ni pamoja na kuhofia kwenda shuleni. Rupert Colville msemaji wa ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa amesema Kamishna Mkuu anataka mamlaka kuimarisha ulinzi kwa watu wote wenye ulemavu wa ngozi kwenye maeneo yote yenye mashambulizi na kuwafikisha mbele ya sheria wahusika wote, na kuhakikisha kwamba matibabu na huduma kwa wahanga na familia zao vinapatiwa kipaumbele. Nchini Malawi pekee matukio sita yameripotiwa wiki kumi za mwanzo wa mwaka huu ilihali nchini Tanzania tukio la hivi karibini ni la tarehe saba Machi ambapo mtoto wa kiume Baraka Rusambo alishambuliwa na kukatwa kiganja chake. Nchini Burundi albino 19 wameuawa tangu mwaka 2008 na tukio la karibuni zaidi ni la tarehe 12 Disemba mwaka 2014.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)