TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Jeshi la Libya lashambulia waasi mjini Tripoli

Jeshi la Libya lashambulia waasi mjini Tripoli Ndege za kivita za jeshi la Libya mapema leo zimeshambulia ngome za waasi katika uwanja wa ndege wa Tripoli na kuna habari kwamba jeshi hilo linapanga kufanya mashambulizi kama hayo katika uwanja wa ndege mjini Misrata. Habari zinasema kuwa, mashambulizi hayo ni ulipizaji kisasi kwa shambulizi lililofanywa na kundi la waasi la Fajr dhidi ya uwanja mdogo wa ndege wa Zintan. Kamanda wa jeshi la anga la serikali, Saqir El-jaroshi amesema shambulizi dhidi ya ngome ya waasi katika uwanja wa Maitiga mjini Tripoli umeharibu silaha nyingi za waasi hao ingawa hakusema iwapo kumekuwa na maafa au majeruhi. Hujuma za serikali dhidi ya ngome za waasi wa Fajr nchini Libya zimetekelezwa siku chache baada ya kuteuliwa jenerali mustaafu, Khalifa Haftar kuwa mkuu wa majeshi ya nchi hiyo. Haftar amesema kibarua chake ni kuhakikisha waasi hao wanashindwa na kwamba serikali inayotambuliwa kimataifa inarejea mjini Tripoli. Kwa sasa serikali hiyo inaendesha shughuli zake katika mji wa Tobruk ulioko mashariki mwa nchi baada ya waasi wa Fajr kuliteka jiji la Tripoli na kuunda serikali yao hapo.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)