TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Mkuu mpya wa polisi Kenya aidhinishwa

Joseph Boinett Kamati za usalama katika mabunge mawili ya nchini Kenya zimeidhinisha uteuzi wa Joseph Boinett kama Inspekta mkuu mpya wa polisi nchini humo. Mwenyekiti wa kamati ya bunge la kitaifa inayohusika na masuala ya usalama, Athman Kamama amesema kamati yake imefanya uchunguzi wa kina na kuridhia Boinett kuwa Inspekta Mkuu mpya wa Polisi. Naye mwenye kiti wa kamati kama hiyo katika bunge la Seneti, Yusuf Haji amesema Boinett anazo sifa zinazohitajika kwa kazi aliyoteuliwa kuifanya. Hapo kesho wabunge wa mabunge hayo mawili watampigia kura Bw. Boinett na iwapo watamauidhinisha, jina lake litawasilishwa kwa Rais Uhuru Kenyatta ili amteue rasmi. Jina la Boinett lilipendekezwa baada ya kujiuzulu Inspekta mkuu wa zamani wa polisi, David Kimaiyo mwishoni mwa mwaka jana.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)