TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

IMF kuipa Sierra Leone fedha ipambane na Ebola

IMF kuipa Sierra Leone fedha ipambane na Ebola Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) umetangaza kuwa utaipa Sierra Leone takriban dola milioni 187 ili kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa Ebola pamoja na kufufua uchumi wake. Dola milioni 80 zitatumika kupambana na Ebola huku fedha zingine zikitumika kuimarisha uchumi. Ahadi hiyo ya IMF imetolewa huko mjini Geneva, Uswisi kunakofanyika mkutano wa kimataifa wa kujadili njia na mikakati ya kupambana na ugonjwa hatari wa Ebola. Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya Ebola, David Nabarro amesema, kibarua kikubwa kilichopo mbele ya viongozi wa dunia ni kuhakikisha ugonjwa huo unatokomezwa kabisa. Marais wa nchi tatu za magharibi mwa Afrika zilizoathiriwa pakubwa na ugonjwa huo wanahudhuria mkutano wa Geneva. Takwimu zinaonyesha kuwa, hadi sasa takriban watu 10,000 wamepoteza maisha kutokana na ugonjwa wa Ebola wengi wao wakiwa ni kutoka nchi za Guinea, Sierra Leone na Liberia. 
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)