 
     
    Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema kuwa, Muswada wa 
Marekebisho ya Sheria mbalimbali likiwemo suala la Mahakama ya Kadhi, 
utawasilishwa katika Bunge lijalo ukiwa na maudhui ya kuangalia jinsi ya
 kuendesha masuala ya imani ya dini ya Kiislamu. Akizungumza na 
waandishi wa habari mjini Dar es Salaam, Mizengo Pinda amebainisha 
kwamba, serikali imeridhia kupelekwa kwake baada ya kuwepo maridhiano 
baina ya makundi mawili ya dini za Kikristo na Waislamu juu ya 
uendeshwaji wa mahakama hiyo. Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema kama 
ninavyomnukuu: “jambo hilo tunalolipeleka Bungeni tunataka tuweke 
utaratibu wa kulitambua, kwa kuwa jambo hili linaloombwa na upande wa 
pili ni la kusaidia utekelezaji wa maamuzi yao na sio kuingilia masuala 
ya jinai, na ni vyema tuone umuhimu wake”. Waziri Mkuu Pinda ameongeza 
kuwa, katika muswada huo wenye maeneo 14, Mahakama ya Kadhi ni sehemu ya
 tano katika sheria hiyo na kwamba, mapendekezo yake ni pamoja na 
kuangalia sheria ya mwaka 1964 inayotamka suala la Uislamu litazamwe na 
lirekebishwe na kuja na mawazo yatakayoweka vipengele vitakavyowezesha 
mahakama kuamua mambo yao.
 
                            About 
                            NELSON PASCHAL KAMUGISHA
 
                            This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
                          
 
 
 
0 comments:
Post a Comment