TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Mahakama ya Kadhi Tanzania kurejeshwa Bungeni

Mahakama ya Kadhi Tanzania kurejeshwa Bungeni Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema kuwa, Muswada wa Marekebisho ya Sheria mbalimbali likiwemo suala la Mahakama ya Kadhi, utawasilishwa katika Bunge lijalo ukiwa na maudhui ya kuangalia jinsi ya kuendesha masuala ya imani ya dini ya Kiislamu. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Dar es Salaam, Mizengo Pinda amebainisha kwamba, serikali imeridhia kupelekwa kwake baada ya kuwepo maridhiano baina ya makundi mawili ya dini za Kikristo na Waislamu juu ya uendeshwaji wa mahakama hiyo. Waziri Mkuu Mizengo Pinda amesema kama ninavyomnukuu: “jambo hilo tunalolipeleka Bungeni tunataka tuweke utaratibu wa kulitambua, kwa kuwa jambo hili linaloombwa na upande wa pili ni la kusaidia utekelezaji wa maamuzi yao na sio kuingilia masuala ya jinai, na ni vyema tuone umuhimu wake”. Waziri Mkuu Pinda ameongeza kuwa, katika muswada huo wenye maeneo 14, Mahakama ya Kadhi ni sehemu ya tano katika sheria hiyo na kwamba, mapendekezo yake ni pamoja na kuangalia sheria ya mwaka 1964 inayotamka suala la Uislamu litazamwe na lirekebishwe na kuja na mawazo yatakayoweka vipengele vitakavyowezesha mahakama kuamua mambo yao.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)