TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

TZ yaomboleza raia 42 waliofariki katika ajali ya gari

TZ yaomboleza raia 42 waliofariki katika ajali ya gari Viongozi mbalimbali wa Tanzania wameendelea kutuma salamu za rambirambi kufuatia msiba mkubwa uliolikumba taifa hilo la Afrika Mashariki baada ya watu wasiopungua 42 kufariki dunia katika ajali ya barabarani hapo jana mkoani Iringa. Rais Jakaya Kikwete amewaongoza Watanzania kuomboleza vifo vya raia wenzao waliopoteza maisha baada ya kutokea ajali mbaya ya barabarani. Rais Jakaya Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa, na kuwahakikishia wafiwa wote kuwa yuko pamoja nao na kuwaombea majeruhi wote wapone haraka ili waendelee na shughuli zao za ujenzi wa taifa. Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bi Amina Masenza amesema katika salamu zake za rambirambi kama ninavyomnukuu: “msiba huu ni wa watu wote, siyo wa mtu mmoja, nimesikitika sana kusikia kuwa asubuhi kuna ajali ilitokea  eneo la Changarawe nje kidogo ya mji wa Mafinga, na niliposikia nimekuja mara moja kuangalia ni jinsi gani tutafanya ili kuwasaidia ndugu hawa.” Zaidi ya watu 42 walipoteza maisha katika ajali hiyo ya jana huko Mafinga Mkoani Iringa. Ajali hiyo ilihusisha lori la mizigo na basi la abiria ambalo kufuatia ajali hiyo liliangukiwa na Kontena na kulikandamiza.

Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)