Viongozi mbalimbali wa Tanzania
wameendelea kutuma salamu za rambirambi kufuatia msiba mkubwa
uliolikumba taifa hilo la Afrika Mashariki baada ya watu wasiopungua 42
kufariki dunia katika ajali ya barabarani hapo jana mkoani Iringa. Rais
Jakaya Kikwete amewaongoza Watanzania kuomboleza vifo vya raia wenzao
waliopoteza maisha baada ya kutokea ajali mbaya ya barabarani. Rais
Jakaya Kikwete ametuma salamu za rambirambi kwa Mkuu wa Mkoa wa Iringa,
na kuwahakikishia wafiwa wote kuwa yuko pamoja nao na kuwaombea majeruhi
wote wapone haraka ili waendelee na shughuli zao za ujenzi wa taifa.
Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Bi Amina Masenza amesema katika salamu zake za
rambirambi kama ninavyomnukuu: “msiba huu ni wa watu wote, siyo wa mtu
mmoja, nimesikitika sana kusikia kuwa asubuhi kuna ajali ilitokea eneo
la Changarawe nje kidogo ya mji wa Mafinga, na niliposikia nimekuja mara
moja kuangalia ni jinsi gani tutafanya ili kuwasaidia ndugu hawa.”
Zaidi ya watu 42 walipoteza maisha katika ajali hiyo ya jana huko
Mafinga Mkoani Iringa. Ajali hiyo ilihusisha lori la mizigo na basi la
abiria ambalo kufuatia ajali hiyo liliangukiwa na Kontena na
kulikandamiza.
0 comments:
Post a Comment