TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Rais Kenyatta: Sitowalinda viongozi mafisadi Kenya

Rais Kenyatta: Sitowalinda viongozi mafisadi Kenya Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema kuwa hana nia ya kuwakingia kifua maafisa wanaojihusisha na ufisadi ndani ya serikali yake.
Kiongozi huyo amesema uchunguzi unaoendelea kuhusu sakata la ‘kuku’ unapaswa kuharakishwa na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria. Imedaiwa kuwa maafisa waandamizi wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) na Baraza Kuu la Mitihani (KNEC) walipokea hongo kutoka kwa kampuni moja ya uchapishaji nchini Uingereza ili kuipa kampuni hiyo zabuni ya kuchapisha makaratasi ya uchaguzi na mitihani miaka miwili iliyopita. Waziri mmoja wa serikali ya sasa pia anatuhumiwa kuhusika na kashfa hiyo ya mamilion ya fedha ambayo inajulikana kama ‘kashfa ya kuku’
“Rais hana nia ya kumlinda mtu yeyote hata kama ni waziri na anachosubiri ni matokeo ya uchunguzi unaoendeshwa na Tume ya Kupambana na Ufisadi” amesema afisa mmoja wa ikulu ya Nairobi ambaye hakutaka jina lake litajwe. 
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)