TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Rambirambi zaendelea kutolewa kifo cha Komba

Rambirambi zaendelea kutolewa kifo cha Komba Viongozi mbalimbali nchini Tanzania wameendelea kutoa salamu za rambirambi kwa familia ya mbunge wa Mbinga Magharibi, Kapteni John Komba, aliyefariki dunia hapo jana. Rais Jakaya Kikwete amesema taifa limempoteza kiongozi shupavu na aliyekuwa na moyo wa kuwahudumia wananchi hususan watu wake wa Mbinga Magharibi. Rais Kikwete amesema marehemu Komba alikuwa muumini wa utawala wa sheria na uadilifu na kwamba kifo chake ni pigo kubwa kwa taifa na Chama Cha Mapinduzi (CCM). Spika wa Bunge, Bi. Anna Makinda amesema Bunge limempoteza mwanachama jasiri aliyesimamia haki na kueleza wazi misimamo yake bila ya woga.
Mbunge huyo alifariki dunia hapo jana punde baada ya kufikishwa katika hospitali ya TMJ jijini Dar es Salaam baada kupata maumivu ghafla akiwa nyumbani kwake.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)