TENGENEZA BLOG BOMBA SASA..

Mahakama Misri: Sheria za uchaguzi hazipo sahihi

Mahakama Misri: Sheria za uchaguzi hazipo sahihi Mahakama Kuu ya Katiba ya Misri imeasema kuwa baadhi ya sehemu za sheria ya uchaguzi ya nchi hiyo zinakinzana na katiba ya nchi. Mahakama hiyo leo imepinga ibara moja katika sheria ya uchaguzi ya Misri ambayo inazigawa wilaya za uchaguzi kwa ajili ya uchaguzi ujao wa bunge. Mahakama Kuu ya Katiba ya Misri hivi sasa inapasa iamue iwapo uchaguzi wa bunge uliopangwa kufanyika Machi 21 uakhirishwe au la. Mohamed Abdel Wahhab, mmoja wa mawakili ambaye amepinga sheria ya uchaguzi ya Misri amesema kuwa, uchaguzi wa bunge utaakhirishwa na kwamba mchakato unapaswa kuanza tangu mwanzo. Pia Rais wa Misri ameamuru sheria hiyo ya uchaguzi iandikiwe rasimu katika kipindi cha chini ya mwezi mmoja akisema kuwa hatua zote za kisheria zinapasa kuchukuliwa ili kuepuka kuakhirishwa uchaguzi wa bunge nchini humo. Itakumbukwa kuwa mwaka 2012, mahakama hiyohiyo yaani Mahakama Kuu ya Katiba ya Misri ililivunja bunge ambalo wakati huo lilikuwa linadhibitiwa na harakati ya Ikhwanul Muslimin ikidai kuwa, bunge hilo halikuchaguliwa kwa mujibu wa katiba.
Share on Google Plus

About NELSON PASCHAL KAMUGISHA

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment

CREATED AND DESIGNED BY NELLYPAKA(WWW.NELLYPAKA.BLOGSPOT.COM)